Serikali ya Kenya yamtimua Koffi Olomide Kwa kumpiga mnenguaji wake wa kike
Serikali ya Kenya mapema leo imechukua uamuzi wa kumtimua mwanamuziki kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Koffi Olomide kufuatia tukio alilolifanya jana la kumpiga mnenguaji wake wa kike katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi.
Taarifa
za kuaminika kutoka jijini Nairobi zimeeleza kuwa Koffi Olomide
alikamatwa na polisi jana majira ya saa nne usiku alipotoka kufanya
mahojiano na Citizen TV.
Mwanasheria
wa Koffi Ollomide, Prof George Wajackyah amesema kuwa tangu
walipokamatwa jana usiku walitunzwa kama wanyama na kwamba Serikali ya
Kenya imewatimua na kuwarudisha Congo hata bila kuwa na passport zao.
Alisema
walitimuliwa kwa nguvu na kusindikizwa leo asubuhi hata bila kupewa
nafasi ya kwenda mahakamani Jumatatu kama walivyokuwa wanatarajia.
Koffi Olomide alitua nchini humo jana akitarajia kufanya tamasha kubwa leo lakini limeota mabawa.
Jeshi
la mitandao ya kijamii la Wakenya ambalo linatajwa kuwa na nguvu zaidi
Afrika Mashariki hasa kupitia twitter kuanzia jana lilimshambulia vikali
Koffi Olomide kwa hatua yake ya kumtwanga teke mnenguaji wake jijini
Nairobi, katika tukio ambalo lilinaswa kwenye kamera.
Serikali ya Kenya yamtimua Koffi Olomide Kwa kumpiga mnenguaji wake wa kike
Reviewed by WANGOFIRA
on
09:33:00
Rating:
No comments: