Samia ataka Afrika iunganishe nguvu kudhibiti uhalifu
MAKAMU wa Rais, Samia Hassan Suluhu, amezitaka nchi za Afrika
kuunganisha nguvu kudhibiti uhalifu ukiwemo ugaidi, utekaji nyara,
biashara haramu ya binadamu na dawa za kulevya.
Samia alisema hivyo juzi, baada ya kuwatunuku watendaji mbalimbali
katika sekta ya ulinzi kutoka nchi za Afrika, waliopata Stashahada na
Shahada ya Uzamili katika Usalama na Strategia kutoka Chuo cha Ulinzi wa
Taifa (NDC).
Akitunuku shahada hizo, alisema ushirikiano katika masuala ya usalama
unazidi kukua kwa nchi rafiki na Tanzania, baada ya watendaji wa
masuala hayo kupata elimu katika chuo hicho cha taifa.
Alisema, watendaji kutoka nchi za Botswana, Burundi, Kenya, Malawi,
Namibia, Nigeria, Afrika Kusini, Zambia, Zimbambwe na China wamejumuika
katika kupata mafunzo kutoka chuo hicho jambo linaloonesha kuendelea
kukuza ushirikiano.
“Tunaweza na lazima kufanya kazi kwa pamoja ili kujenga nguvu na
umoja dhidi ya wahalifu katika nyanja zote na si ushirikiano katika
silaha pekee, lakini pia kwa kutumia akili zetu kuweka mikakati ya
kukabiliana nao,” alisema Samia.
Alieleza kuwa kwa kuhakikisha nchi hizo zinafanya kazi pamoja ni
vyema pia kutumia busara kwani kuwepo mataifa mbalimbali katika kumaliza
shahada hiyo ya usalama ni ishara tosha kuwa vitendo vya uhalifu na
ugaidi inahitaji ushirikiano kutoka kwa nchi zote jirani.
Pia aliwataka wahitimu hao kutoka nchi mbalimbali kuhakikisha elimu
waliyopata inawasaidia katika kufanikisha kuhakikisha nchi hizo
zinafanya kazi kwa pamoja huku wakiwa mabalozi wa chuo hicho katika nchi
zao.
Akizungumza katika mahafali hayo, Mkuu wa Chuo cha NDC, Meja Jenerali
Yakub Mohamed, alisema katika mahafali hayo wanafunzi 39 waliohitimu
masomo, 22 walipata Shahada ya Uzamili na 17 Stashahada ya Usalama na
Strategia.
HABARI LEO
Samia ataka Afrika iunganishe nguvu kudhibiti uhalifu
Reviewed by WANGOFIRA
on
20:56:00
Rating:
No comments: