Sababu Iliyomfanya Mgana Msindai Kurudi Tena CCM Baada ya Kuhamia CHADEMA

Aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida na baadaye kuhama chama na kujiunga na CHADEMA, Mgana Msindai ametangaza kurudi CCM.

Msindai alitangaza uamuzi huo jana mjini Dodoma baada ya kupewa nafasi na Mwenyekiti Mstaafu wa CCM, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete wakati anaendesha mkutano mkuu wa CCM uliomchagua Rais Dk John Magufuli kuongoza chama.

Msindai alisema aliamua kurudi CCM baada ya kuona kuwa sasa hakuna cha kupinga baada ya Rais Magufuli kuchaguliwa kuwa rais wa nchi.

Msindai aliingia CHADEMA baada ya aliyekuwa mgombea wa Ukawa, Edward Lowassa kujiunga na Chadema mwaka jana wakati wa uchaguzi mkuu.
Sababu Iliyomfanya Mgana Msindai Kurudi Tena CCM Baada ya Kuhamia CHADEMA Sababu Iliyomfanya Mgana Msindai Kurudi Tena CCM Baada ya Kuhamia CHADEMA Reviewed by WANGOFIRA on 20:40:00 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.