Sababu Iliyomfanya Mgana Msindai Kurudi Tena CCM Baada ya Kuhamia CHADEMA
Aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida na baadaye kuhama chama na kujiunga na CHADEMA, Mgana Msindai ametangaza kurudi CCM.
Msindai alitangaza uamuzi huo jana mjini Dodoma baada ya kupewa nafasi
na Mwenyekiti Mstaafu wa CCM, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete wakati
anaendesha mkutano mkuu wa CCM uliomchagua Rais Dk John Magufuli
kuongoza chama.
Msindai alisema aliamua kurudi CCM baada ya kuona kuwa sasa hakuna cha
kupinga baada ya Rais Magufuli kuchaguliwa kuwa rais wa nchi.
Msindai aliingia CHADEMA baada ya aliyekuwa mgombea wa Ukawa, Edward
Lowassa kujiunga na Chadema mwaka jana wakati wa uchaguzi mkuu.
Sababu Iliyomfanya Mgana Msindai Kurudi Tena CCM Baada ya Kuhamia CHADEMA
Reviewed by WANGOFIRA
on
20:40:00
Rating:
No comments: