Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amempokea Mhe. Paul Kagame wa Rwanda leo Jijini Dar
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amempokea Mhe. Paul Kagame Rais wa Jamhuri ya Rwanda kwa ziara rasmi ya kiserikali. Rais Magufuli ameambatana na Mkewe Mama Janeth Magufuli na Rais Kagame ameambatana na mkewe Mama Jeannette Kagame. Ziara hii ni ya siku mbili.Baada ya Hapo ataelekea Ikulu jijini Dar es Salaam kwa ajili ya Kufanya Mazungumzo.
Baada
ya hapo wataelekea katika Viwanja vya Maonesho ya Kimataifa ya Sabasaba
jijini Dar es Salaam kwa ajili ya ufunguzi rasmi ya maonesho ya 40 ya
Kimataifa katika viwanja vya Sabasaba leo.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aakiwa
ameambatana na mgeni wake Mhe. Paul Kagame Rais wa Jamhuri ya Rwanda
mara baada ya kuwasili asubuhi hii katika uwanja wa ndege wa Kimataifa
wa Julius Nyerere kwa ziara rasmi ya siku mbili ya kiserikali. Rais
Magufuli ameambatana na Mkewe Mama Janeth Magufuli na Rais Kagame
ameambatana na mkewe Mama Jeannette Kagame.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na
mgeni wake Mhe. Paul Kagame Rais wa Jamhuri ya Rwanda wakipata Gwaride
la heshima uwanjani
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na
mgeni wake Mhe. Paul Kagame Rais wa Jamhuri ya Rwanda wakitazama kikundi
cha ngoma za asili kilichokuwa kikitumbuiza uwanjani hapo.
Rais Paul Kagame akiwapungia mkono baadhi ya wananchi mbalimbali waliofika kumlaki uwanjani hapo,kushoto kwake ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.
PICHA ZOTE KWA HISANI YA IKULU.
PICHA ZOTE KWA HISANI YA IKULU.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amempokea Mhe. Paul Kagame wa Rwanda leo Jijini Dar
Reviewed by WANGOFIRA
on
08:18:00
Rating:
No comments: