NDIKILO: WAKATI WA PROPAGANDA UMEISHA TUFANYE KAZI
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo
Na Mwamvua Mwinyi, Pwani
MKUU wa mkoa wa Pwani mhandisi Evarist Ndikilo,
ametoa rai kwa wananchi mkoani humo kuungana kwa pamoja na serikali ya awamu ya
tano kufanya kazi ili kuinua uchumi na maendeleo ya mkoa na Taifa kijumla.
Aidha amesema wakati wa malumbano ya kisiasa na
propaganda umekwisha hivyo jamii iwe nyuma ya mh Rais Magufuli na serikali yake
kujenga maendeleo ya nchi.
Akizungumza mara baada ya kupokea taarifa ya tume ya
uchaguzi kutoka kwa afisa uchaguzi tume ya Taifa ya uchaguzi, Adam Nyando, mkuu
huyo wa mkoa alisema wakati wa kukaa na kuzungumzia itikadi za kisiasa
umekwisha kilichobaki ni kukubaliana na matokeo yaliyotangazwa na sio
vinginevyo.
"Walioshinda wameshinda, aliyekosa kakosa, maji
yameshamwagika, lakini kwa watanzania wote tumeshinda kwa kuwa tuna amani
"
"Nawasihi wote tuungane kufanya kazi ili kuleta
maendeleo ya Taifa, tuchape kazi ili yote yaliyoahidiwa wakati wa uchaguzi
yapate nafasi kutekelezwa" alisema mhandisi Ndikilo.
Hata hivyo mhandisi Ndikilo alielezea kuwa kijumla
mkoani Pwani zoezi la uchaguzi mkuu lilikwenda vizuri hadi kipindi cha
kutangazwa kwa matokeo.
Alisema wapo baadhi ya watu walisema na kufikiri
nchi isingetoka salama na ingetumbukia kwenye machafuko ya kisiasa baada ya
uchaguzi mkuu badala yake hali ipo shwari.
Alisema mungu alituepushia na kutuondoa huko na sasa
tupo shwariiii huku CCM ikiwa imeshinda ambapo Rais wa nchi ni John Magufuli.
Mhandisi Ndikilo alieleza baadhi ya nchi huwa
wakitumbukia kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe, uvunjifu wa amani ama vurugu
nyakati za uchaguzi hivyo kwa Tanzania haina budi kumshukuru mungu kwa
kutuvusha na kuendelea kuwa na amani.
Awali akimkabidhi mkuu wa mkoa huyo taarifa ya tume
ya uchaguzi afisa tume ya Taifa ya uchaguzi, Adam Nyando, alisema kwa sasa tume
ya uchaguzi inajielekeza kufanya majukumu mbalimbali ikiwemo elimu ya mpiga
kura na zoezi la uandikishaji wapiga kura.
Alisema majukumu hayo yataenda sambamba na
maandalizi ya mchakato wa kura ya maoni kwa kuanzia na kurekebisha sheria ya
kura ya maoni.
Akieliza anasema uchaguzi mkuu umemalizika kwa amani
na utulivu hivyo tume inaendelea na majukumu yake mengine kwa maslahi ya Taifa.
Hata hivyo alielezea kuwa zoezi la uandikishaji
wapiga kura utakuwa ni endelevu.
Nyando alisema sheria inasema kati ya uchaguzi mmoja
na uchaguzi mwingine lazima kuwe na uandikishaji unaofanyika.
Mratibu wa uchaguzi mkoani Pwani, Shangwe Twamala,
alisema changamoto zilizojitokeza katika uchaguzi mkuu 2015 zitashughulikiwa
mapema kabla ya chaguzi zijazo.
Katika Uchaguzi mkuu uliopita CCM ilishinda majimbo
yote 9 ya mkoani Pwani na Rais na makamu wa Rais Samia Suluhu walishinda kwa
kupata kura nyingi dhidi ya vyama vingine vya upinzani.
NDIKILO: WAKATI WA PROPAGANDA UMEISHA TUFANYE KAZI
Reviewed by WANGOFIRA
on
20:09:00
Rating:
No comments: