MSEVENI ASIMAMISHA MSAFARA ILI AONGEE NA SIMU.


Rais wa Uganda bwana Yoweri Kaguta Museveni amezua kioja katika kijiji kimoja karibu na mpaka wa Uganda na Tanzania .


Je ushawahi kupokea simu ya dharura ?

Je wewe hujitenga vipi na watu waliokaribu nawe ima ni mkeo ama hata wafanyakazi wenza iliupokee simu ya kibinafsi?

Na je katika enzi hizi za simu za kisasa au Smartphone wangapi wetu wanatumia simu za kale zisizo na touchscreen ?

Haya basi,
Museveni hata aliwapungia mkono wapita njia 

Hayo sio maswali ya kipima joto,,,la!

Rais wa Uganda bwana Yoweri Kaguta Museveni alizua kihoja katika kijiji kimoja karibu na mpaka wa Uganda na Tanzania aliposimamisha msafara wake wa magari iliapokee simu faraghani.

Amini usiamini Rais Yoweri Museveni, alishuka kutoka kwenye gari lake rasmi akachukua kiti chake na kukiweka kando kando ya barabara mpya ya Isingiro ikipitia kijiji hicho cha Kyeirumba hadi Tanzania na kupokea simu faraghani.

Wenyeji walifurahia kuwa na mgeni ambaye hawakumtarajia 

Mzee Museveni kama vile baba wa taifa alitumia muda wake kufanya shughuli hiyo huku akiwapungia mkoo wapita njia.

Baada ya dakika 30 hivi raia wa kijiji hicho walishangaa kuwa miongoni mwa maafisa wakuu serikalini.

Wenyeji walikuwa na la kumweleza kiongozi huyo wa taifa 

Ilikuwa ajabu sana kwao kumuoana Museveni akiwa ameketi barabarani.

Waganda katika mitandao ya kijamii wamesambaza picha hiyo ya rais museveni akizungumza kwa simu ambayo inaonekana kuwa sio ya kisasa.


Je wewe hujitenga vipi na watu waliokaribu nawe ima ni mkeo ama hata wafanyakazi wenza iliupokee simu ya kibinafsi? 

Wengine wanamkejeli kwa kuhofia kudukuliwa huku wengine wakimgoa kwa kuketi barabrani

''kwani hangeweza kupokea simu yake ndani ya gari lake ?

''ni siri gani hiyo ambayo hakutaka hata walinzi wake wasikie,

''Ama ilikuwa ni #Besigyexit ? wakizungumzia kuachiliwa kwa dhamana kwa kiongozi wa upinzani Kizza Besigye.

Via>>BBC
MSEVENI ASIMAMISHA MSAFARA ILI AONGEE NA SIMU. MSEVENI ASIMAMISHA MSAFARA ILI AONGEE NA SIMU. Reviewed by WANGOFIRA on 20:48:00 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.