Maiti Yazuiliwa hospitali ya Muhimbili ikidaiwa fedha


Hospitali ya Taifa Muhimbili imegoma kuruhusu mwili wa marehemu Bi Hilda Lukas miaka 30 aliyefariki dunia June 26 katika hospitali hiyo, akisumbuliwa na ugonjwa wa utumbo kutoboka huku ikidai lazima fedha yote wanayomdai marehemu ilipwe ambayo ni sawa na shilingi milioni moja na laki moja na nusu kwa mujibu wa ndugu wa familia kama gharama za kumuhudumia mgonjwa huyo.
 
Mama wa marehemu Bi Anna Zuaro na Bibi wa marehemu wameiomba serikali na wadau mbalimbali kuona namna wanavyoweza kuwasaidia kwani wao mpaka sasa hawana fedha za kuuondoa mwili wa mpendwa wao, huku gharama za kuuhifadhi mwili huo katika chumba cha kuhifadhi maiti zikizidi kuongezeka.
 
Maafisaa wa Muhimbili wanakiri marehemu Hilda Lukas alikuwa amelazwa katika wodi ya kibasira chumba namba 9 ingawa haikuwa rahisi kuzungumza na maafisa hao.
 
Uongozi wa mtaa wa Chang’ombe umesema umefanya juhudi nyingi tu zikiwemo za kuchangisha wananchi na wadau mablimbali lakini mpaka sasa bado hawajaweza kukamilisha kiasi hicho cha fedha kinachohitajika Muhimbili ambapo gharama za mochwari pekee mpka sasa ni shilingi 210,000.
Maiti Yazuiliwa hospitali ya Muhimbili ikidaiwa fedha Maiti Yazuiliwa hospitali ya Muhimbili ikidaiwa fedha Reviewed by WANGOFIRA on 20:36:00 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.