FAIDA ZA KUNYONYA VIDOLE KWA WATOTO
Ripoti mpya inasema watoto
wanaonyonya vidole au kung'ata kucha zao kwa meno huenda wasipate
matatizo ya kuathirika kutokana na mazingira hewa au kula vyakula
fulani.
Kwa mujibu wa waandishi katika jarida la Pediatrics, huo
ni ni usafi dhanio,kwani yatokanayo na baadhi ya wadudu huimarisha mfumo
wa kinga ya mwili.
Unyonyaji wa kidole gumba na ung’ataji wa kucha umeonekana kuzuia baadhi ya alergy.
Kati
ya watu elfu moja wenye umri wa kati ya miaka mitano hadi thelathini
na mbili,walifanyiwa uchunguzi kwa muda nchini New Zealand.
Lakini tabia hii ya unyonyaji vidole na ung’ataji kucha haisaidii watu wenye pumu au mtu anapopata homa kali.
Uchunguzi
uliofanywa na kurekodiwa kwa watoto wenye umri wa kati ya miaka mitano
na kumi na moja na wengine waliofanyiwa vipimo ni wenye umri kati ya
miaka kumi na tatu na thelathini na miwili.
Huku thuluthi moja ya
watoto hao ni wanyonyaji wa vidole mara kwa mara au hung’ata kucha zao
na katika vipimo walivyofanyiwa watoto hao wameonekana kuwa wana kiwango
kidogo cha kuathirika kutokana na mazingira hewa au kula vyakula
fulani
Watoto wanaoweza kupata matatizo ya kuathirika
kutokana na mazingira hewa au kula vyakula fulani (alergy) kutokana na
vitu kama vumbi kutoka majumbani,manyoya ya paka au mbwa, lakini watoto
wenye kunyonya vidole gumba na kung’ata kucha walikuwa ni chini ya
theluthi moja kuliko watoto wenye tabia hii ya unyonywaji vidole.
Na tabia hii ya unyonyaji vidole au ung’ataji kucha inaonekana kuwa kinga mpaka wanapofikia umri wa utu uzima.
"
kuwa na paka au mbwa majumbani,ndugu au jamaa wanaofanya kazi
mashambani pia imeonekana kuwa ni sababu kubwa inayosababisha mazingira
ya ukuaji wa magonjwa yanayosababishwa na
kuathirika kutokana na mazingira hewa au kula vyakula fulani
CHANZO; BBC
FAIDA ZA KUNYONYA VIDOLE KWA WATOTO
Reviewed by WANGOFIRA
on
06:36:00
Rating:
No comments: