Donald Trump akubali uteuzi wake
Donald Trump ameahidi kukomesha
matukio ya uhalifu na vurugu nchini Marekani endapo atafanikiwa kuwa
rais mteule wa taifa hilo, ahadi hii ameitoa kwatika hotuba yake wakati
alipokuwa anathibitisha ukubalifu wake wa kuteuliwa kuwa mgombea urais
kwa tiketi ya chama cha Republican.
Maneno ama ahadi hiyo imo
katika moja ya kifungu cha hotuba yake hii ni baada ya kuvuja kwa hotuba
hiyo na kudakuliwa na wataalamu wa udakuzi na kueleza kuwa hotuba hiyo
imesheheni ahadi tele za ya kurejesha utawala wa sheria , ikiwemo suala
la kukabiliana na uhamiaji haramu na kwamba suala hilo ataliingiza
katika sera za kigeni za Marekani.
Pamoja na hayo Trump anatarajiwa kutoa tamko kuwa
mara moja atahakikisha anasimamia suala la wahamiaji haramu kutokana na
mataifa kuathiriwa na wimbi la masuala ya ugaidi na kusisitiza ahadi
yake ya kujenga ukuta kwenye mpaka baina ya Marekani n a nchi ya Mexico
ili kuondokana na suala la wahamiaji.
Naye mpinzani wa Donald
Trump bibi Hillary Clinton, atathibitishwa juma lijalo kupitia chama
chake cha Democrats ambapo chama hicho kitakuwa mkutano mkubwa katika
jimbo la Philadelphia.
BBC
Donald Trump akubali uteuzi wake
Reviewed by WANGOFIRA
on
20:54:00
Rating:
No comments: