ASSUMPTER MSHAMA AANZA KAZI NA WANAOKUMBATIA ARDHI

Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
MKUU mpya wa wilaya ya Kibaha ,Assumpter Mshama ametoa miezi 6 kwa taasisi mbalimbali na wananchi walio na maeneo makubwa ambayo hawayaendelezi kuyaendeleza katika muda huo na atakaekaidi hati yake itafutwa kwa mujibu wa sheria.
Amesema wapo watu na taasisi mbalimbali ambazo zimekumbatia maeneo makubwa pasipo kuyaendeleza na kuyaacha pori hali inayosababisha kuwa maficho ya kiuhalifu..
Aidha Assumpter amewataka watendaji wa kata,maafisa tarafa  na wakurugenzi wa halmashauri zilizopo wilayani humo kuhakikisha wanakamilisha zoezi la upatikanaji wa madawati  ifikapo July 29 mwaka huu.
Mkuu huyo wa wilaya alitoa maagizo hayo mjini Kibaha kwenye mkutano alioundaa ili kuzungumza masuala mbalimbali ya wilaya kwa watumishi wa halmashauri za wilaya,wakuu wa idara ,maaafisa tarafa na watendaji wa kata .
Assumpter alieleza kuwa mtumishi atakayeshindwa kutekeleza maagizo hayo kwenye sehemu yake ya kazi atakuwa amejifukuzisha kazi mwenyewe.
Alisema hatomfumbia macho mtu ama taasisi yeyote ambayo imechukua maeneo yaliyo umbali wa km.5 kutoka barabara kuu katika kipindi kirefu bila kuyashughulikia.
Hata hivyo Assumper alisema NSSF ina jumla ya eneo lenye hekta 7.5 sawa na hekari 18  huko Mkoani B,ambalo lilichukuliwa kwa ajili ya kujenga makazi lakini halijaendelezwa tangu mwaka 1997 lilipomilikishwa.
“Taasisi za aina hii siwezi kuzikumbatia hata kidogo,ni lazima haki itendeke ,nina msuli nalo jambo hili.Na kuna watu wengine wanakaa katika eneo lile kwa miaka 12 sasa ambapo wanahitajika waondolewe
“alisema Assumpter.
Alisema haiwezekanai taasisi ama mtu anahasi eneo lake kwa bila kulihudumia halafu baada ya miaka 10/20 ndipo anajitokeza na kuondoa wananchi ambabo wameshakaa katika eneo hilo kwa zaidi ya miaka 12.
Alieleza wapo wawekezaji wengi wenye nia ya kuwekeza hivyo ni vyema kuyachukua maeneo hayo yasiyofanyiwa kazi kwa maslahi ya mtu binafsi.
Akizungumzia suala la madawati aliwataka watumishi hao wasilale usiku na mchana ,watafute mbinu za kufikia lengo la idadi ya madawati ambayo yanahitajika wilayani hapo.

Assumpter alisema ni wajibu wa kila mmoja ndani ya jamii kuguswa na suala hilo la kielimu ili kutekeleza agizo la Rais John Magufuli kwa lengo la kuondokana na uhaba wa madawati mashuleni.
Alitoa agizo jingine la kuweka mji safi kuanzia mailmoja Kibaha hadi Mlandizi kwani Mji wa Kibaha upo usoni mwa barabara kuu ya Morogoro.
Kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kibaha Lucy Kimoi,alisema wamepokea maagizo yote na watenda kuyafanyia kazi.
Akitolea ufafanuzi juu ya suala la madawati Lucy alisema ,halmashauri hiyo ilikuwa na upungufu wa madawati katika shule za msingi 9,162 ambapo hadi kufikia June 30 walikuwa tayari wametengeneza na kukarabati madawati 6,979 hivyo kwasasa wana upungufu wa  2,183.
Lucy alisema katika upande wa shule za sekondari mahitaji ya meza yalikuwa 7,032 vilivyopo  ni 6,041 na kubakia na upungufu wa meza 991 huku viti walivyokarabati na kutengeza ni viti 6,099 kukiwa na upungufu wa viti  933 hadi sasa.
Nae afisa ardhi halamashauri ya Mji wa Kibaha,Gilly Simiyu alisema wataendeleza kushughulikia masuala ya migogoro ya ardhi kwa wakati kama walivyoagizwa na mkuu huyo wa wilaya.
Alisema kisheria huwezi kufuta matumizi ya ardhi katika maeneo yanayomilikiwa kihalali kwa urahisi bila kufuata sheria ikiwemo kuwapa taarifa wamiliki kisha kufuata taratibu za kufutiwa hati .

Mwisho
ASSUMPTER MSHAMA AANZA KAZI NA WANAOKUMBATIA ARDHI ASSUMPTER MSHAMA AANZA KAZI NA WANAOKUMBATIA ARDHI Reviewed by WANGOFIRA on 20:54:00 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.