Wizara ya Fedha na Mipango waadhimisha wiki ya Utumishi wa Umma kwa kufanya mkutano
Wizara
ya Fedha na Mipango imeadhimisha wiki ya Utumishi wa Umma kwa kufanya
mkutano na Watumishi wake, lengo likiwa ni kujadili mafanikio na
changamoto wanazo kabiliana nazo mahali pa kazi.
Akizungumza
wakati wa maadhimisho hayo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na
Mipango, Bw. Doto James aliwataka Watumishi kuunga mkono juhudi za
Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. John Magufuli
katika kupambana na masuala ya rushwa, uzembe kazini na Watumishi hewa
ambao wamekuwa wakiigharimu Serikali fedha nyingi katika kutekeleza
majukumu yake ya kuwaletea wananchi maendeleo.
Alisema
Wizara inajipanga kuhakikisha inaboresha mazingira ya kazi kwa
watumishi hasa kwa wale wenye ulemavu kwa kuwajengea miundombinu rafiki
sehemu za kazi ili kuongeza ufanisi kazini.
Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James akizungumza
na wafanyakazi wa wizara hiyo katika maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa
Umma kwenye ukumbi wa mikutano hazina.Kulia ni Mkurugenzi wa Utawala na
Rasilimali watu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Gideon Manambo.
“Wizara
pia inafanya vizuri katika masuala ya usawa wa kijinsia kwa kuwa na
idadi inayoridhisha ya wanawake hasa katika ngazi za maamuzi, ikiwa ni
pamoja na kuwa na Manaibu Katibu Wakuu wawili wanawake” . Alisisitiza
James
Naye
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu wa Wizara ya Fedha na Mipango,
Bw. Gideon Manambo alisema kuwa, watumishi wanatakiwa kufanya kazi kwa
ufanisi na kwa bidii ili kuendana na kasi ya mabadiliko ya maendeleo
ambayo yanahitaji watendaji wenye weledi wa kutosha ili kukabiliana na
changamoto zinazojitokeza.
Kwa
upande wa watumishi wa Wizara, wameuomba uongozi kuhakikisha kunakuwepo
na vitendea kazi vya kutosha ili waweze kufanya kazi kwa ufanisi na
kuwa na matokeo chanya ambayo yatasaidia kutatua matatizo yanayowakabili
wananchi.
Maadhimisho
hayo yamefanyika kufuatia utaratibu mpya uliowekwa na Serikali ya Awamu
ya Tano ambapo uliagiza Wizara pamoja na Taasisi kuadhimisha Wiki hiyo
kwa kutatua matatizo ya watumishi wa Umma pamoja na wananchi kwa ujumla
katika maeneo yao ya kazi.
Wizara ya Fedha na Mipango waadhimisha wiki ya Utumishi wa Umma kwa kufanya mkutano
Reviewed by WANGOFIRA
on
20:41:00
Rating:
No comments: