Wabunge watatu wa CHADEMA wasimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge
Mbunge
wa Mbeya mjini kwa tiketi ya Chama cha Demokrasi na Maendeleo
(CHADEMA), Joseph Mbilinyi amesimamishwa kuhudhuria na vikao 10 vya
Bunge kuanzia leo kufuatia kitendo cha kuonyesha kidole cha kati bungeni.
Joseph
Mbilinyi alitenda kosa hilo alipokuwa akitoka nje ya ukumbi wa Bunge
baada ya kile alichoeleza kuwa kuna mbunge wa CCM aliyemtusi mama yake.
Hata hivyo alipohojiwa kama anamfahamu mbunge huyo, Mbilinyi alisema
kuwa hamfahamu.
Hukumu
hiyo imesomwa leo na Naibu Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson baada ya
Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Bunge kueleza kuwa kamati hiyo
ilijiridhisha kuwa kitendo kilichofanywa na mbunge huyo kuwa ni kosa.
Aidha
wabunge wangine waliosimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge ni pamoja na
Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo, James Ole Millya Mbunge wa Simanjiro
kwa makosa yanayofanana ya kusema uongo bungeni. Wabunge hawa
wamesimamishwa kuhudhuria vikao vitano kuanzi leo.
Katika
hatua nyingine, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameahirisha mkutano wa tatu
wa Bunge lililokuwa na lengo la kujadili na kupitisha bajeti ya
serikali ya mwaka wa fedha 2016 2017. Kufuatia kuahirishwa huko, kuanzia
kesho Julai Mosi, serikali itaanza kutekeleza miradi na mpango mingine
iliyoanishwa katika bajeti hiyo.
Wabunge watatu wa CHADEMA wasimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge
Reviewed by WANGOFIRA
on
04:32:00
Rating:
No comments: