UKAWA Wamgomea Rais Magufuli.......Wamtaka Aandae Magereza za Kutosha
Mwenyekiti wa Chadema na Kiongozi wa
Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe amesema hawatakubaliana
na kauli ya Rais John Magufuli ya kukataza mikutano ya shughuli za siasa
hadi mwaka 2020 na kama hivyo ndivyo, Serikali iandae magereza ya
kutosha.
Mbowe ambaye pia ni mwenyekiti mwenza wa Ukawa, alisema jana
kuwa kutokana na kauli hiyo kuwa nzito vyama vinavyounda umoja huo
vitakutana na kujadiliana kabla ya kutoa msimamo wa pamoja.
Mbunge huyo
wa Hai alisema wamepokea kwa mshtuko mkubwa kauli na maagizo ya Rais
Magufuli kuhusiana na haki ya kufanya shughuli za kisiasa ikiwamo
mikutano ya hadhara, makongamano na hata maandamano kwa vyama vya siasa.
“Aandae magereza ya kutosha kwa sababu hatutazibwa midomo... kama
wananchi wananyimwa fursa ya kusema ni vibaya, watatumia vitendo mambo
ambayo yalileta vita katika nchi za wenzetu.
"Mbowe alisema Rais Magufuli anastahili kujua siasa siyo starehe, bali ni kazi kama zilivyo nyingine zozote. Alisema siasa siyo tukio la uchaguzi, bali ni maisha ya kila siku na ni mfumo unaogusa maisha ya kila siku.
"Mbowe alisema Rais Magufuli anastahili kujua siasa siyo starehe, bali ni kazi kama zilivyo nyingine zozote. Alisema siasa siyo tukio la uchaguzi, bali ni maisha ya kila siku na ni mfumo unaogusa maisha ya kila siku.
“Uhalali wa kazi za siasa
unatolewa na Katiba aliyoapa kuilinda na kukaziwa na Sheria Namba 5
ya mwaka 1992 (Political Parties Act NO. 5 of 1992) pamoja na
marekebisho yake,” alisema.
Alisema uhalali huo ndiyo unaomfanya yeye
kuwa Rais leo na ndiyo unaotoa uhalali wa chama chake kuwepo na
kutekeleza kihalali na kisheria majukumu yake ya kila siku.
Alisema haki ya kufanya siasa haiwezi kuwa miliki ya Serikali, wabunge na madiwani pekee kama Rais
anavyoagiza.
“Akumbuke uchaguzi mkuu siyo tukio pekee la kisiasa. Kuna
chaguzi za serikali za mitaa, chaguzi za marudio na mambo mengine mengi.
Ni wajibu wa msingi wa vyama vya siasa kufuatilia utendaji kazi wa kila
siku kwa wale wanaoongoza Serikali na hivyo siasa siyo uchaguzi pekee,”
alisema Mbowe.
Alisema elimu ya uraia na ile ya siasa ni wajibu mkuu wa
vyama vya siasa na hustahili kutolewa wakati wote na siyo na wanasiasa
wa kuchaguliwa au kuteuliwa pekee.
“(Rais Magufuli) anapaswa kubaini
kuwa vyama vya siasa vina miundo ya viongozi na watendaji nchi nzima
ambao majukumu yao ni ya muda wote na siyo ya msimu wa uchaguzi pekee,”
alisema.
Alisema makongamano yakiwamo ya siasa anayolalamikia Rais ni
pamoja na Kigoda cha Mwalimu J.K. Nyerere ambalo lilionekana kuhoji
mambo kadhaa yanayogusa mustakabali wa nchi.
“Makongamano katika vyuo na
taasisi mbalimbali ni sehemu muhimu ya taaluma na huibua uelewa
muhimu kwa jamii,” alisema.
Alisema makongamano mengi huandaliwa na
taasisi zisizo za kiserikali na taasisi za dini na kusema Rais
anastahili kutambua kuwa siasa inamgusa kila mmoja kwani ni maisha ya
watu.
Mbowe alisema; “walianza kwa kulithibiti Bunge na wabunge wa
upinzani kwa kujaza askari bungeni kama vile ni uwanja wa vita. Leo ni
vyama vya siasa vya upinzani kupewa likizo ya lazima ya Rais; kesho
inaweza ikawa taasisi za dini, baadaye asasi zisizokuwa za kiserikali na
hatimaye nchi hii itaweza kugeuka nchi ya utawala wa mabavu ya kutumia
dola,” alisema na kuongeza:
“Ukawa hatutakubaliana na hali hii. Hili ni
tamko la hatari kwa demokrasia, utawala wa sheria, haki za binadamu na
linakinzana na kila aina ya uhuru ambao Katiba yetu aliyoapa kuilinda
Rais, imetoa.”
Aliwataka Watanzania wote wakatae utamaduni huu mpya
ambao alisema utabomoa mshikamano wetu kama Taifa.
Mbowe alisema Rais kuwa mkali katika kusimamia uwajibikaji na utendaji wa Serikali ni jambo jema lakini linapoteza maana kama ukali huo unatumika kuvunja Katiba na sheria na kuziba watu midomo.
Mbowe alisema Rais kuwa mkali katika kusimamia uwajibikaji na utendaji wa Serikali ni jambo jema lakini linapoteza maana kama ukali huo unatumika kuvunja Katiba na sheria na kuziba watu midomo.
“Uhuru ni jambo la kupigania na kutetea
kwa gharama yoyote ile na tuko tayari kwa wajibu huo. Wanaoweza
kumshauri Rais na wafanye hivyo kwani athari za jambo hili likiachiwa
likaota mizizi, hata hayo maendeleo anayoyapigania yanaweza kubaki kuwa
ndoto na nchi kuingizwa kwenye machafuko yasiyo ya lazima,” alisema.
James Mbatia
Msimamo kama huo pia ulitolewa na Mwenyekiti Mwenza wa
Ukawa, James Mbatia aliyesema Rais ameweka kando Katiba.
Mbatia ambaye
pia ni Mbunge wa Vunjo (NCCR- Mageuzi), alisema kauli nyingi ambazo
zimekuwa zikitolewa na Rais zimekuwa hazizai matunda na kutoa mfano wa
kuzuia sukari kutoka nje ya nchi kuingia nchini jambo ambalo muda mfupi
baadaye, ilibainika kuwa sukari ya nchini haitoshelezi mahitaji.
“Hatuombi ruhusa kwa Rais kufanya mikutano ya kisiasa, bali ni haki yetu
kikatiba,” alisema.
Mbunge wa Viti Maalumu (CUF), Riziki Ng’wale,
alisema kauli ya Rais Magufuli si sahihi kwa sababu siasa ni kazi na
hakuna namna anavyoweza kuweka wigo wa kuyafanya mambo hayo.
“Kwa sisi
wakongwe wa siasa tunamwambia apanue magereza, hatutakubali hilo...
Aache ubabe,” alisema.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanataaluma wa Vyuo
Vikuu na Vyuo Vikuu Vishiriki vya Umma nchini, (ASA), Paul Louslie
alisema agizo la Rais Magufuli ni gumu kutekelezeka hata ndani ya CCM.
“Kukaa bila kukutana kwa vyama vya siasa hata ndani ya CCM labda kwa
sababu yeye ni Mwenyekiti wa CCM na ni Amiri Jeshi Mkuu. Na hapo akiamua
kutumia madaraka yake hatatenda haki kwa vyama vingine vya kisiasa,”
alisema.
Alisema kazi ya siasa ni kukutana na watu na haiwezekani kukaa
ndani bila kukutana na watu kwa muda wote kwani huko ni kuua chama.
UKAWA Wamgomea Rais Magufuli.......Wamtaka Aandae Magereza za Kutosha
Reviewed by WANGOFIRA
on
20:50:00
Rating:
No comments: