SIKU YA MTOTO WA AFRIKA ILIVYOFANA KATIKA VIWANJA VYA JAKAYA KIKWETE YOUTH PARK
JAMII imetakiwa kubadilika kwa kuacha
kufanya ukatili wa watoto ili kuweza kuwa na watoto kwa kujitambua. Hayo
ameyasema leo Mkugenzi Mtendaji wa Taasisi isiyo ya Kiserikali C-SEMA,
Kiiya Joel, wakati wa maadhimisho ya siku mtoto wa Afrika iliyofanyika
katika viwanja vya Jakaya Kikwete, amesema kesi nyingi za watoto
kutelekezwa ambazo zimekuwa zikifikia kituomn hicho kupitia huduma ya
simu mkononi.
Kiiya amesema watoto wanatelekezwa na kufanya watoto
kuishi mitaani na kuhitaji msaada wa kujikimu hali ambayo inafanya
watoto kukosa haki ikiwemo kukosa elimu.
Amesema kuwa katika utoaji wa huduma ya simu C-SEMA imejipanga
kuboresha huduma visiwani Zanzibar ili kuhakikisha vitendo viovu vya
watoto vinapatiwa taarifa. “Tumepata fedha ambazo C sema itaboresha
huduma kupiga ya simu kwa ajili ya kupata matukio ambayo yanakandamiza
watoto visiwani Zanzibar “, amesema Kiiya.
Na amewataka watanzania
kutoa ushirikiano kwa kupiga simu ya bure 116 na kutoa taarifa za
matukio ya ukatili dhidi ya watoto ili yaweze kutatuliwa mara
moja. Watoto katika picha ya Pamoja .
Amesema kuwa kituo cha huduma ya simu kwa mtoto kimekuwa hakipokei
simu nyingi kutokana na kwamba huduma hiyo haijafahamika maeneo mengi
ambapo kwa mwezi hupokea simu 30 kiwango ambacho ni kidogo kulingana na
ukubwa wa tatizo.
“Naomba watanzania wote popote pale walipo kupiga simu
ya bure 116 pale wanaposikia taarifa za kuwepo kwa matukio ya ukatili
dhidi ya watoto ili yaweze kufanyiwa kazi,” amesema
Amesema kuwa toka
kituo hicho kianze Juni 16, mwaka 2013 wamekuwa wakipokea simu za
matukio ya watoto kupewa ujauzito, matunzo ya watoto baada ya
kutekelezwa, ulawiti na ubakaji.
Read More
SIKU YA MTOTO WA AFRIKA ILIVYOFANA KATIKA VIWANJA VYA JAKAYA KIKWETE YOUTH PARK
Reviewed by WANGOFIRA
on
06:18:00
Rating:
No comments: