Mwingine Akamatwa kwa Kumtukana Rais JPM Kupitia "WhatsApp"

Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi,ambapo mtu  mwingine ameingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais kwenye mtandao wa WhatsApp.

Mtuhumiwa huyo aliyefahamika kwa jina la Leonaard Mulokozi Kyaruzi ameshtakiwa chini sheria ya uhalifu wa mtandaoni (Cybercrime act) ya mwaka 2015. 

Huyu anakuwa ni mtu wa pili kushtakiwa baada ya wa kwanza kufikishwa mahakamani mkoani Arusha kwa kumtukana Rais Magufuli kwenye mtandao wa Facebook.

Kyaruzi ujumbe wake unasomeka hivi. "Hivi huyu Pombe ni kwamba hana washauri? Hashauri? Au ni zuzu? Bwege sana huyu jamaa, he doesn’t consider the law in place before opening his mouth!. Au na yeye anaumwa ugonwja wa mnyika?”

Hii hapa ni hati ya shtaka linalomkabili Kyaruzi.
Mwingine Akamatwa kwa Kumtukana Rais JPM Kupitia "WhatsApp" Mwingine Akamatwa kwa Kumtukana Rais JPM Kupitia "WhatsApp" Reviewed by WANGOFIRA on 20:54:00 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.