MERCY KITOMARI: MJASIRIAMALI KIJANA ANAYEFIKIRIA MAKUBWA
Mjasiriamali kijana Mercy Kitomari akiwa ofisini kwake wakati wa mahojiano.
Modewjiblog ilipata
bahati ya kuzungumza ana kwa ana na Mercy Kitomari mmoja wa
wajasiriamali wanawake vijana ambaye anafikiria kuwa na kiwanda kikubwa
cha ashkrimu (ice cream) ifikapo mwaka 2020 akizisafirisha na kuziuza
Tanzania nzima na Afrika Mashariki. Wapi alipotokea, yuko wapi kwa sasa,
ni machungu gani aliyokumbana nayo na anaishauri nini serikali na
wajasiriamali wenzake. Haya yote utayajua katika mahojiano haya .Soma…
MODEWJI BLOG: Role model wako nani?
MERCY: Magufuli. You know why?(unajua
kwanini?) ametuweka wazi kabisa kwamba maisha ni changamoto na
tusikubali kushindwa ni lazima kupambana na kufanyakazi kwa bidii na
maarifa kuondoa vigingi vyote vinavyotukwamisha. Amenifanya nifanye kazi
kwa bidii. Nataka kuwa mwanamke anayefanya mabadiliko. Hakuna kitu
kinachokuja kirahisi. Nataka kuwa mwanamke yule ambaye anaonesha tofauti
nataka kuifanya nchi yangu iniringie.
Sijisikii vibaya kwa kuwa niko mpweke,
kitu cha kwanza ni kazi, nataka kuifanya mwenyewe ili wanawake wenzangu
watambue kwamba tunaweza kufanya wenyewe, bila msaada wa mwanaume. Ndio
unahitaji mume lakini si katika hili suala la ujasiriamali, mwanamke
peke yako unaweza kuleta mabadiliko.
Nataka kuwa mwanamke ambaye Afrika itaniringia na taifa langu litanichekelea kwamba mimi ni binti yao.
MODEWJI BLOG: Turejee katika masuala ya
kodi. Kodi ni muhimu sana kwa mapato ya serikali. Je Kodi zinazowatoza
zinawasaidia au zinawavunja moyo?
MERCY: To be honest (kusema ukweli)
zinatuvunja moyo. Nyingi ya hizi kodi hazitusaidii sisi watu wa hali ya
chini kunyanyuka, zinatukwamisha.Kodi zimewekwa bila kujali madaraja.
Anayeanza na aliyemo, mwenye kipato kidogo na kikubwa. Na yote hayo
yanafanyika bila kuzingatia kwamba kuwapo kwa wajasiriamali wengi ndio
kuchangamka kwa soko la wakulima na pia ajira viwandani.
Mimi ninayetengeneza ashkrimu natengeneza
ajira; ninatengeneza soko kwa yule anayeleta matunda sokoni kwani naenda
kununua matunda kwa ajili ya ashkrimu. Kodi nyingi zinakandamiza,
haziangalii ukubwa na udogo wa biashara. Mtu anabiashara inayoingiza
mamilioni kwa siku anawekwa kundi moja na anayeingiza laki moja.
Muonekano wa nje wa duka la Ice Cream la
Nelwa’s Gelato la Mercy Kitomari lililopo ndani ya Petrol Station ya
SOPCO barabara ya Morogoro-Magomeni Mwembechai karibu na kwa Sheikh
Yahya.
MODEWJI BLOG: Ukikutakana na role model wako utamuomba nini?
MERCY: Nikikutana na Magufuli? Kwanza
naomba nikutane naye! Nikikutana naye nitamwambia ofisi zote za huduma
kwa wananchi ziwe katika mtandao (online) watu tuweze kufanya kila kitu
katika mtandao. Na Serikali za mitaa lazima zirejeshe faida kwa wananchi
kwa kodi zao.
Wanatakiwa watufundishe vitu vingi.
Watufundishe kuwa wajasiriamali namna ya kufunga na kuuza bidhaa zetu
wasifanye tu shughuli za kukusanya ushuru na kodi, watuambie namna ya
kuendelea mbele ili waendelee kukusanya ushuru na kodi au hawatakusanya
kitu tukikwama.
Ni lazima wawekeze kwa wajasiriamali ili kuwepo na hali bora zaidi.
Ukitazama soka katika televisheni unaona
matangazo mengi ya krisp hapa kwetu wapo wadada wanaotembeza za ndizi au
viazi hawa wakifundishwa namna nzuri ya kuweka chakula chao ni dhahiri
tutakuwa na wajasiriamali wengi. Wanatakiwa watuelekeze mambo mengi
bidhaa za kwenye ‘super market’ zinakuaje na kadhalika wasibaki kudai na
kuvuna hela tu watusaidie tuweze kuwapatia fedha zaidi. Lakini nambieni
lini nitakutana na role model wangu huyu…….ha ha ha ha….kicheko….!
MODEWJI BLOG: Wasaidizi wake wakisoma
makala haya watajua nini unahitaji na pasi shaka watakukutanisha naye.Ni
watu wema hawa, hawawezi kukosa kukupangia muda wa kumuona Role Model
wako umweleze mambo ya kukusaidia wewe na wengine wa aina yako.
MERCY: Nakudai hilo kwani natamani sana
atukutanishe wanawake vijana wajasiriamali ili azungumze nasi. Najua
ameshazungumza na wafanyabiashara wakubwa, lakini akituona na sisi
atatambua uwezo wetu na namna ambavyo angetusaidia tungeibuka wengi na
kuweka ndoto ya Tanzania ya viwanda katika ukweli.
You know (unajua) nilikutana na wanawake
wenzetu wajasiriamali kutoka Uganda na Rwanda naona wameendelea
kwelikweli na siri ni serikali zao kuhakikisha kwamba wanaendelea.
Wapo wanawake waliokata tamaa hapa,
nimekutana nao nikasema tusichoke hata kidogo serikali ya sasa inataka
viwanda ni lazima kuisaidia kujua tunawezaje kufikia ndoto hiyo, kuna
vizingiti hapa wakiviondoa tutaweza.
KWA HISANI YA MODEWJI BLOG.
MERCY KITOMARI: MJASIRIAMALI KIJANA ANAYEFIKIRIA MAKUBWA
Reviewed by WANGOFIRA
on
07:14:00
Rating:
No comments: