JWTZ Yakanusha Taarifa za Kuibwa kwa Kifaru
Jeshi
la wananchi wa Tanzania (JWTZ) limekanusha taarifa za kuibiwa kwa
kifaru cha jeshi zilizoripotiwa leo na gazeti la Dira na kusema kuwa
taarifa hizo hazina ukweli wowowte huku likisisitiza ulinzi katika
maeneo ya jeshi uko imara.
Akiongea na waandishi wa habari leo kukanusha habari hizo, msemaji wa jeshi hilo, Kanali Ngemela Lubinga amesema jeshi limesikitishwa sana na habari hizo za upotoshaji kwa kuwa zinachafua taswira ya jeshi na taifa kwa ujumla.
Amelitaka Gazeti la Dira kuomba radhi mara moja na wakishindwa kufanya hivyo hatua Kali na za kinidhamu zitachukuliwa dhidi yao Akiongea na waandishi wa habari leo kukanusha habari hizo, msemaji wa jeshi hilo, Kanali Ngemela Lubinga amesema jeshi limesikitishwa sana na habari hizo za upotoshaji kwa kuwa zinachafua taswira ya jeshi na taifa kwa ujumla.
TAZAMA HAPA VIDEO BOFYA HAPA KUIONA
JWTZ Yakanusha Taarifa za Kuibwa kwa Kifaru
Reviewed by WANGOFIRA
on
20:25:00
Rating:
No comments: