Halmashauri nchini zatakiwa kutokuwa wabadhirifu wa fedha za miradi
Halmashauri
nchini zatakiwa kufanya kazi kwa weledi na ufanisi ili kuleta matokeo
chanya na kwa wakati, huku wakijiepusha na ufujaji rasilimali za umma
wakati wa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.
Hayo
yamebainishwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na
Serikaliza Mitaa (OR-TAMISEMI) Mhandisi Mussa Iyombe alipokuwa
akimwakilisha Waziri wa nchi OR – TAMISEMI Mhe. George Simbachawene
katika uzinduzi rasmi wa mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Hali ya
Hewa na Tabia nchi (Decentralized Climate Finance in Tanzania) jana mjini Dodoma.
“Niseme
tu kuwa nategemea utendaji wenye matokeo chanya kwa kufanya hiyvo
kutajenga imani kwa wafadhili, Wakurugenzi wote nchini fanyeni kazi kwa
weledi,ufanisi na muepuke kufuja mali za umma” Alisema Mhandisi Iyombe.
Katibu
Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI)
Mhandisi Mussa Iyombe akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa mradi
Kukabiliana na Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabia nchi (Decentralized
Climate Finance in Tanzania) jana mjini Dodoma.
Mhandisi
Iyombe aliongeza kuwa mradi huu umelenga kuwajengea uwezo wanajamii
katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya hali ya hewa na tabia nchi
ambapo juhudi mbalimbali zimekuwa zikifanyika katika kukabiliana na
hilo.
Serikali
kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo hususan Shirika la Kimataifa la
Mazingira na Maendeleo (IIED), Haki Kazi Catalyst (HKC), Jumuiko la
Maliasili Tanzania(TNRF) chini ya ufadhili wa Serikali ya Uingereza
(UK-aid) na Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo (UNCDF LoCAL)
itatekeleza mradi huu katka Halmashauri 15 nchini.
Halmashauri
hizo ni pamoja na Kondoa, Bahi, Manyoni, Mpwapwa, Kiteto, Same,
Simanjiro, Kilwa, Siha, Mbulu, Iramba na Pangani ambazo zimejumuishwa na
Halmashauri za Monduli, Ngorongoro na Longido zilizokuwa katika mradi
wa majaribio.
Naibu
Katibu Mkuu anayeshughulikia Afya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) Dkt. Deo Mtasiwa akizungumza wakati wa
hafla ya uzinduzi wa mradi Kukabiliana na Mabadiliko ya Hali ya Hewa na
Tabia nchi (Decentralized Climate Finance in Tanzania) jana mjini
Dodoma.
Kwa
upande wake Naibu Katibu Mkuu anyeshughulikia Afya kutoka OR-TAMISEMI
Deo Mtasiwa amesema kuwa kwakuwa Serikali tayari imekwisha tengeneza
mfumo imara ilikuhakikisha utekelezaji wa mradi huo unafanikiwa kuanzia
ngazi ya kijiji.
Akizungumza
wakati wa uzinduzi wa mradi huu MwakilishiMshauri wa Taasisi ya
Kimataifa ya Mazingira na Maendeleo (IIED) Alais Morindat alisema kuwa
mabadiliko ya hali ya hewa siyo kitu kipya na kuongeza kuwa historia ya
mradi huo inatokana na athari zilizojitokeza katika jamii za wafugaji
katika maeneo ya Kasikazini mwa Tanzania ambapo mifugo mingi katika
maeneo ya Monduli, Ngorongoro na Longido ilipoteza uhai.
Meneja
Miradi wa Mfuko wa Umoja wa Taifa wa Maendeleo (UNCDF) Bw. Fakri Karim
akiwasilisha mada namna mfuko wao unavyoshiriki katika mradi wa
Kukabiliana na Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabia nchi (Decentralized
Climate Finance in Tanzania) wakat wa uzinduzi wa mradi huo mjini
Dodoma.
MwakilishiMshauri
wa Taasisi ya Kimataifa ya Mazingira na Maendeleo (IIED), Alais
Morindat akielezea chimbuko la mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya
Hali ya Hewa na Tabia nchi (Decentralized Climate Finance in Tanzania)
wakati wa uzinduzi wa mradi huo mjini Dodoma.
Baadhi
ya wadu wadau wa mradi wa Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabia nchi
akiwemo mwakilishi wa mtandao wa wanahabari watoto wanaoshughulika na
mabadiliko ya tabia nchi Bi. Getrude Clement (16) mwenye tisheti ya
kijani wakifuatilia mada wakati wa uzinduzi wa mradi huo leo mjini
Dodoma.
Katibu
Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI)
Mhandisi Mussa Iyombe (watano kutoka kushoto) akiwa katika picha ya
pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo katika uzinduzi wa mradi wa
Kukabiliana na Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabia nchi (Decentralized
Climate Finance in Tanzania) mjini Dodoma. (Picha na: Nasra Mwangamilo,
TAMISEMI).
Halmashauri nchini zatakiwa kutokuwa wabadhirifu wa fedha za miradi
Reviewed by WANGOFIRA
on
20:44:00
Rating:
No comments: