Askari Polisi Mwanza Matatani Kwa Kudaiwa Kusababisha Kifo cha Mganga wa Jadi
Familia
ya marehemu Daniel Lumondo, mkazi wa kijiji cha Kalundye wilaya ya
Nkasi mkoani Rukwa, imelishutumu jeshi la polisi mkoani Mwanza kwa madai
ya kusababisha kifo cha ndugu yao, baada ya askari polisi wa kituo cha
Kirumba wilayani Ilemela kumtia nguvuni kwa tuhuma za kujipatia fedha
kiasi cha shilingi milioni moja kwa njia za udanganyifu.
Marehemu
Lumondo ambaye wakati wa uhai wake alikuwa akijishughulisha na tiba
asili katika eneo la Kirumba jijini Mwanza, alifariki dunia Juni 14
mwaka huu majira ya saa tisa usiku katika hospitali ya rufaa Bugando
alikokuwa amelazwa kwa muda wa siku nne kwenye chumba cha wagonjwa
mahtuti, chini ya ulinzi mkali wa polisi ambao walimkamata Juni 4 mwaka
huu kwa tuhuma za madai ya kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu toka
kwa Ferdinand Mtazi mkazi wa Jijini Mwanza.
Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi Ahmed Msangi amethibitisha tukio hilo na kuongeza kwamba jeshi hilo linamshikilia askari wake mmoja kwa mahojiano na uchunguzi zaidi wa kifo hicho.
Hili ni tukio la pili kwa askari polisi kuhusishwa na vifo vya watuhumiwa wa makosa mbalimbali, ambapo mwezi Aprili mwaka huu askari polisi watatu wa kituo cha polisi Muleba mkoani Kagera walidaiwa kumpiga na kumsababisha kifo mvuvi mmoja wa kisiwa cha Kunene wilaya ya Ukerewe mkoani Mwanza Hamis Tabibu Kilangi na mpaka sasa hakuna hatua zozote za kinidhamu na kisheria zilizowahi kuchukuliwa na Jeshi hilo dhidi ya askari hao.
Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi Ahmed Msangi amethibitisha tukio hilo na kuongeza kwamba jeshi hilo linamshikilia askari wake mmoja kwa mahojiano na uchunguzi zaidi wa kifo hicho.
Hili ni tukio la pili kwa askari polisi kuhusishwa na vifo vya watuhumiwa wa makosa mbalimbali, ambapo mwezi Aprili mwaka huu askari polisi watatu wa kituo cha polisi Muleba mkoani Kagera walidaiwa kumpiga na kumsababisha kifo mvuvi mmoja wa kisiwa cha Kunene wilaya ya Ukerewe mkoani Mwanza Hamis Tabibu Kilangi na mpaka sasa hakuna hatua zozote za kinidhamu na kisheria zilizowahi kuchukuliwa na Jeshi hilo dhidi ya askari hao.
Via>>ITV
Askari Polisi Mwanza Matatani Kwa Kudaiwa Kusababisha Kifo cha Mganga wa Jadi
Reviewed by WANGOFIRA
on
20:13:00
Rating:
No comments: