PROF. NDALICHAKO, HESLB BADO KUNA MAJIPU YA MENGI.
BARAKA NGOFIRA
Unaweza
kushangaa na kuhuzunishwa na vijana wa kitanzania hasa wale watoto wa maskini
waliokosa mikopo huku wakiwa na sifa za kupewa mikopo hiyo. Pia waweza kuona
kuwa wanaonewa pale watoto wa wenye navyo kupewa vipaumbele nap engine kupewa
aslimia mia moja za mkopo.
Sishangai
maana hii ni hali ya kawaida hasa kwa mataifa mengi ya kiafrika ambapo Rushwa
na kujuana kumetawala miongoni mwa viongozi na ulafi wa madaraka, na undugu
kutalawa na kuweka nyuma ubinadamu wa watu wengine.
Pia
hata sishangai kuona watoto wa yule mkulima, mfugaji na mwalimu wa shule ya msingi aliyedharauliwa,
kutojaliwa katika haki zake za msingi ikiwemo elimu na Afya.
Pia
sioni shida yoyote watoto wa wenye navyo waliozoea kula mkate wa blue band na
chai ya maziwa kila kuchapo, huku mlangoni gari la shule likipiga honi
kuwaita kwenda shule kupewa mkopo tena kwa asilimia mia moja. Lakini mtoto wa
maskini anayeshindia viazi na mihogo ya kuchoma kila siku kukosa mkopo kwa
sababu ya fani anayosoma eti haina kipaumbele.
Haya
ni maisha ya kawaida, kwetu watoto wa masikini ambao hatujui kesho yetu
itakuwaje. Lakini nikiwa mdogo nakumbuka wazazi wangu walinifunza kuridhika na
maisha ya kwetu, bila shaka naamini wenzangu na mimi hawa nao walifundishwa
vivyo hivyo.
Ndio
maana hata hawashangai kunyanyaswa na wakubwa wachache waliokalia ofisi
zilizojawa na viyoyozi na viti vya magurudumu wakizunguka bila shida. Ni
kawaida lakini maana hata kwenye vitabu vitakatifu wameandika mwenye nacho
uongezewa na asiyenacho unyang’anywa hata kile alichonacho.
Naandika
makala hii kwa niaba ya wanafunzi wenzangu tuliodahiliwa mwaka wa masomo
2014/2015 katika vyuo mbalimbali hapa nchini, lakini hatukupewa mikopo na bodi
ya mikopo kwa kile tulichoambiwa kuwa “Badget exhausted” yaani bajeti ya
serikali kwa mwaka wa fedha 2014/15 haitoshi kuwapa wanafunzi wote wenye vigezo
vya kupata mkopo.
Na
kuahidiwa kuwa serikali itakapopata fedha tutazingatiwa kwanza, lakini
makubaliano hayakuwa kama tulivyokubaliana maana fedha zilivyokuja tuliwaona
watoto wa matajiri wakiongezewa mikopo na baadhi yao waliokuwa hawajapewa nao
ikawa nafasi yao ya kunufaika.
Hatukukata
tamaa kwenda ofisi ya bodi ya mikopo kuuliza tatizo liko wapi maana fedha
zimekuja na tulioambiwa tutanufaika kuwekwa pembeni. Majibu tuliyopewa
yalitufedhehesha na kulaumu kuzaliwa kwenye familia maskini. Lakini kwa sababu
hatukupenda kuzaliwa huko tulijikaza tu maana hakuna namna nyingine zaidi ya
kuvumilia kuendelea kuishi kwa mkate na maji kila siku.
Lakini
baada ya kuona tumefedheheshwa na majibu yao walituambia tujaribu kuomba tena
kwa mwaka wa fedha 2015/16, huenda tukapewa, lakini mambo yakawa ni yaleyale.
Tulijipa
moyo na kuendelea maisha ya chuo kwa wazazi wetu kukopa fedha nyingi kwenye
vikoba, na kwenye mabenki halikuisha. Ambapo mpaka sasa wanadaiwa fedha nyingi
na naamini muda si mrefu dhamana zao walizoweka zikiwemo hati za nyumba
mashamba, viwanja na dhamana nyingine karibu zipigwe mnada kwa ajili ya
kushindwa kulipa madeni makubwa wanayodaiwa mpaka sasa kwa ajili ya kutupigania
watoto wao tusome.
Lakini kwa sasa maji yametufika shingoni tena
maji ya barafu damu zishatuganda, na wengine wameshaacha masomo kwa kukosa ada
na fedha za kujikimu, kwa upande wa dada zetu baadhi yao kwa sababu ya upeo
mdogo wa kufikiri wameshageuza bidhaa za kuuza miili yao vichochoroni ili tu
waweze kuyamudu maisha ya chuo.
Ukiachilia
mbali hayo, mwanzoni mwa mwezi wa pili mwaka huu watendaji wanne wa bodi ya
mikopo walisimamishwa kazi kwa matumizi mabaya ya madaraka. ambapo jambo liliotuhumiza zaidi ni pale
tuliposikia zaidi ya wanafunzi 54,000 walipewa mikopo bila kuomba. Na wengine
zaidi ya 5000 kupewa mikopo huku majina yao yakiwa kwenye zaidi ya chuo kimoja.
Japo
hatua hiyo ilipongezwa na wanafunzi wengi ambao walikuwa hawajapata mikopo kwa
matumaini ya kwamba huenda tulioahidiwa kunufaika na mikopo kwa kudanganywa
kuandika majina lakini bado mambo ni yaleyale.
Rai yangu
kwako Mama yetu mpendwa nahisi na wewe ulizaliwa familia kama za kwetu za
wazazi oye aye japo kwa kipindi hicho ninyi mlifaidi maana mlipata fursa ya
kusomeshwa bure na serkali yetu tukufu, na kupewa kila kitu .
Najua
unafahamu fika maisha ya chuo jinsi yalivyo urahisi wake na ugumu wake
unaufahamu fika, maana wewe huu msomi na ni imani yangu kuwa Rais wetu mtukufu
hakukosea kukuweka kwenye wizara hiyo ambayo viatu vyake umevivaa vilivyo na
havijakupwaya na wala havitakupwaya kamwe.
Tusaidie tupate nasi mikopo, maana wengi wetu
wamesitisha masomo kwa kukosa mikopo ya
elimu ya juu.
Makala
hii imeandaliwa na Baraka Ngofira, mwanafunzi wa mwaka wa pili chuo nkikuu cha
Dar es salaam anasomea shahada ya kwanza ya mawasiliano nkwa Umma anapatokana
kwa mawasiliano ya 0763580901, au barua pepe ya barakangofira@gmail.com.
PROF. NDALICHAKO, HESLB BADO KUNA MAJIPU YA MENGI.
Reviewed by WANGOFIRA
on
06:23:00
Rating: