MWALIMU MBARONI KWA KUSABABISHA MIMBA


 
Mwalimu wa Shule ya Msingi Nyaigabo iliyopo Kijiji cha Musati wilayani Serengeti, Mkoa wa Mara anatuhumiwa kumsababishia kijana anayemuuzia duka kwa kumpelekea mwanafunzi na kusababisha apate ujauzito. 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Ramadhan Ng’hazi alisema mwalimu huyo, Agness Matiko amekamatwa na kuhojiwa kwa tuhuma hizo. 

Ng’hanzi alisema binti huyo mwenye umri wa miaka 16 alimaliza darasa la saba mwaka jana kwenye shule anayofundisha mwalimu huyo. 

Alisema mwalimu huyo alikuwa akimtoa darasani mwanafunzi na kumpeleka nyumbani kwake na kumkutanisha na kijana wake huyo kwa ajili ya kufanya naye ngono. 

Binti huyo alikuwa anasoma kidato cha kwanza katika Shule ya Sekondari Ikorongo kabla ya kufukuzwa baada ya kubainika kuwa na mimba ya miezi sita. 

“Mwaka jana nikiwa darasa la saba mwalimu alinipeleka nyumbani kwake ili nikamsaidie kukamua ng’ombe maziwa, siku ya pili wakati wa mapumziko alinichukua nikamuoshee vyombo tulimkuta huyo kijana baadaye mwalimu alinisihi nibaki naye ndani,” alidai. 

Alidai licha ya kukataa kufanya naye ngono, lakini mwalimu alimwambia: “Mimi ni mwalimu wako, kama lingekuwa jambo baya nisingekushauri, hivyo wewe kubali, akatufungia kwa nje. Huyo kijana akanipeleka chumbani kwake akanilaza kitandani na kuniingilia.” 

Kwa mujibu wa mwanafunzi huyo baadaye mwalimu huyo alikwenda kufungua mlango na kumchukua na kumpeleka darasani na huo ukawa mwendelezo wa kumkutanisha na kijana huyo. Alidai kila mara alimpeleka nyumbani kwake na kuwakutanisha huku akimwambia anataka waoane. 

“Baada ya kubainika nina ujauzito walimtorosha huyo kijana na kudai kuwa walimfukuza kwa madai aliwatia hasara dukani,” alidai. 

Akizungumza baada ya kupata dhamana, licha ya kukiri kukamatwa kwa tuhuma hizo, mwalimu Matiko alisema hajawahi kumfanyia ukuwadi mwanafunzi huyo. 

Alisema kijana aliyekuwa akiishi kwake walimpata kijijini hapa akiwa anatafuta kazi. “Ndipo tulimpatia kazi ya kuuza duka tangu Aprili hadi Oktoba 2015 nilipomfukuza kwa kunisababishia hasara na alisema kwao ni Mabatini mkoani Mwanza,” alisema. 

Baba wa binti huyo, Marwa Nchama (53) alisema baada ya kubaini ana mimba alifuatilia na kubaini mwanaye alikuwa akifanyiwa vitendo vya unyanyasaji na kijana huyo. 

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Turuka Samwel alikana kulifahamu tukio hilo likiwamo suala la walimu kuwafanyisha kazi wanafunzi majumbani mwao. 

Mkuu wa Wilaya hiyo, Maftah Ally, alisema watumishi wanaohusishwa na tuhuma za kuwapa mimba wanafunzi licha ya kufikishwa mahakamani, watawachukulia hatua za kinidhamu.
MWALIMU MBARONI KWA KUSABABISHA MIMBA MWALIMU MBARONI KWA KUSABABISHA MIMBA Reviewed by WANGOFIRA on 02:59:00 Rating: 5
Powered by Blogger.