MKURUGENZI WA SMART CODES TANZANIA ATAJWA KWENYE ORODHA YA VIJANA 30 WENYE MIAKA CHINI YA 30 YA FORBES AFRICA.
Bwana Edwin Bruno, mjasiriamali wa
Kitanzania, mshindi wa tuzo ya kijana mwenye mafanikio 2015, mwanzilishi
na mkurugenzi wa kampuni ya Smart Codes ametajwa katika jarida la
Forbes Africa. Kila mwaka, jarida hilo hutoa orodha ya vijana 30 wenye
umri chini ya miaka 30 ambao wana nafasi ya kuwa mabilionea wa baadaye.
Majina hayo yalikusanywa na kuandaliwa na
mhariri wa Forbes Afrika, Ancillar Mangena ambaye naye ana chini ya
miaka 30. Katika ujumbe wake, anaandika “Orodha inawakilisha vijana
ambao tunaamini wana uwezo wa siku moja kuwa kwenye ukurasa wa mbele wa
jarida la FORBES AFRICA, ikimaanisha watakuwa na thamani halisi ya si
chini ya dola za kimarekani milioni 200, wameajiri maelfu ya watu na
kusaidia kukua bara la Afrika.”
Katika mazungumzo mafupi na Edwin Bruno,
anasema “Nimepewa heshima kubwa kuwa kwenye orodha hiyo, hata hivyo hii
inatokana na juhudi za timu nzima pale Smart Codes. Ni wao ndio
wanaofanya kazi kubwa, ambayo inaonekana ndani nan je ya nchi”
Kuhusu mafanikio yake mengine, Bruno
anasema “ Ni kweli, mwaka jana programu yetu ya m-paper, ambayo inakupa
nafasi ya kusoma magazeti ya Tanzania…sio vichwa vya habari, ila gazeti
lote kutokea ukurasa wa kwanza hadi wa mwisho kwenye simu yako au
kompyuta ilishinda tuzo ya Best Educatinal Innovation Africa, au kwa
Kiswahili tuzo ya uvumbuzi bora wa kielimu barani Afrika.”
Bwana Bruno alimalizia kwa kuonesha
furaha yake na kuwasihi vijana wengine kufanya kazi kwa kujituma ili
waweze kufikia malengo yao au kama yale aliyosema mhariri wa Forbes
Africa Ancillar, kusaidia kukua kwa bara la Afrika kiuchumi.
MKURUGENZI WA SMART CODES TANZANIA ATAJWA KWENYE ORODHA YA VIJANA 30 WENYE MIAKA CHINI YA 30 YA FORBES AFRICA.
Reviewed by WANGOFIRA
on
20:49:00
Rating: