KIWANDA CHA BIA YA SERENGETI CHAPIGWA FAINI KWA UCHAFUZI WA MAZINGIRA.
Kiwanda cha
bia aina ya serengeti kilichopo chang'ombe wilaya ya Temeke jijini Dar es
salaam kimepigwa faini ya shillingi za kitanzania millioni kumi na sita(16) na
Baraza la usimamizi wa mazingira Nchini (NEMC) baada ya kutokutimiza masharti ya
sheria ya mazingira ya mwaka (2004) na kanuni zake.
Uamuzi huo umefikiwa baada ya Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa raisi
Muungano na mazingira Mh.Luhaga Mpina kupata malalamiko kutoka kwa wananchi
wanaozunguka maeneo ya kiwanda hicho. Na kuainisha uchafuzi wa mazingira yanayowazunguka
wananchi hao yanayohatarisha usalama wa
afya zao.
Na kumlazimu naibu waziri huyo kufanya ziara ya
kushtukiza kiwandani hapo, akiwa ameambatana
na Wakurugenzi kutoka Baraza la usimamizi wa mazingira nchini (NEMC) na
kujionea uharibifu huo.
Mh.Mpina ameagiza kiwanda hicho kulipa faini hiyo na
kurekebisha miundo mbinu hiyo ndani ya siku arobaini na tano kusiwepo tena na utiririshaji
maji machafu na yenye kemikali kali za sumu ambayo yanatoa harufu mbaya
inayohatarisha afya za wakazi wa
chang'ombe wilaya ya temeke.
Pia mkurugenzi wa mazingira Bw. Boniventure Baya
ametoa siku saba kwa kiwanda hicho kiwe kimelipa faini hiyo vinginevyo hatua
kali za kisheria zitachukuliwa kwani wamekua wakikaidi maagizo yanayotolewa na
Baraza hilo la mazingira nchini (NEMC). Na kuwataka kufanya hivyo haraka
iwezekanavyo baada ya kukiuka sheria ya utunzaji mazingira ya mwaka(2004) na
kutokutimiza masharti waliyopewa takribani miaka miwili iliyopita.
Naye mbunge wa Temeke (CUF) Mh.Abdallah Mtolea
alisema kiwanda hicho kimekua na mahusiano mabaya na wananchi wanaozunguka maeneo jirani na kiwanda hicho hivyo kupelekea
kuwa na mgogoro wa muda mrefu na uongozi kiwanda hicho.
Na kumuomba Naibu waziri kutatua
tatizo hilo ambalo limekua likifanywa kwa makusudi na uongozi wa kiwanda hicho
ilihali wanajua madhara ya wanayoyapata wananchi.
Aidha kwa upande wake Afisa mazingira wa kiwanda
hicho Bw.Simon Peter alipinga vikali tuhuma hizo ambazo zimeelekezwa katika
kiwanda hicho na kusema uongozi wa kiwanda hicho unafanya kila jitihada ili
kuweza kutatua kero hiyo na si kweli kwamba hawashughulikii tatizo hilo la
mazingira jirani na wakazi hao.
Kwa upande wa wananchi kupitia kwa Bi.Emanuela
Peter, walisema hiyo ni kero kubwa sana kwao.
Ambapo imekuwa ikiwalazimu kuyahama makazi yao hasa wakati wa kipindi
cha masika, ambapo maji ya mvua na yale ya kiwanda huchanganyikana na kujaza
uchafu wote majumbani mwao hali inayowalazimu kuhamia kwenye nyumba za kulala wageni
kwa muda, hivyo wameiomba serikali kuangalia kwa makini na kuweza kulipatia
ufumbuzi.
Vilevile, Mh.Luhaga alifanya ziara ya kushtukiza katika
kiwanda cha Cement Wazo kilichopo Tegeta wilaya ya kinondoni jijini Dar es
salaam, ambapo hakufanikiwa kuonana na uongozi wa kiwanda hicho kwa madai ya
kuwa nje ya jiji la Dar es salaam. Ambapo alitoa tamko la serikali kuwa, serikali
ya awamu ya tano haina uadui na wafanyabiashara pamoja na wawekezaji kama
inavyozaniwa na watu wengine, bali inachowataka ni kufuatwa kwa Sheria, taratibu
na kanuni kama inavyostahili.
KIWANDA CHA BIA YA SERENGETI CHAPIGWA FAINI KWA UCHAFUZI WA MAZINGIRA.
Reviewed by WANGOFIRA
on
08:57:00
Rating:
No comments: