Bodi ya TCU yavunjwa kutokana na kupitisha majina ya wanafunzi wasiokuwa na vigezo.


Serikali imievunja bodi ya tume ya vyuo vikuu nchini (TCU) huku mwenyekiti wake Hawadhi Mang’enywa ambaye mamlaka ya uteuzi wake yanatokana na rais John Pombe Magufuli akiridhia asimamishwe kazi baada ya kubainika bodi hiyo kupitisha majina ya wanafunzi 486 kusoma shahada ya ualimu chuo kikuu cha mtakatifu Joseph kampasi ya Arusha na Songea huku wakiwa hawana vigezo na baadhi yao wakinufaika na mikopo ya elimu ya juu.

Waziri wa elimu sayansi na teknolojia Joyce Ndalichako amesema uamuzi huo umefikiwa baada ya wanafuzni waliokuwa wakisoma katika chuo hicho kuhamishwa katika vyuo vingine na kubainika kuwa hawana uwezo ndipo uchunguzi juu yao ukafanyika ambapo kati yao 486 walibainika elimu yao kuwa ya kidato cha nne na ufaulu wao ukiwa juu ya alama 32 ambao hawastahili hata kusomea fani hiyo kwa ngazi ya cheti.
Kufuatia bodi hiyo ya TCU kuvunjwa huku shughuli zake ziendelee kufanya kazi ikiwemo udahili wa wanafunzi Mhe Ndalichako amewateua kwa muda Profesa Eliuther Mwageni kukaimu nafasi ya katibu mtendaji na Kokubelwa Katunzi Mollel kumaimu nafasi ya ukiurugenzi wa udahili na nyaraka.
Aidha Mhe Ndalichako ametumia nafasi hiyo kubainisha kuwa wizara imebaini uwepo wa wanafunzi hewa katika vyuo vikuu nchini ambao wamekuwa wakichukua fedha za mikopo ya elimu ya juu kinyume na taratibu ambapo hatua kali zitachukuliwa kwa chuo chochote kitakachobainika kuhusika na mchezo huo mchafu.
Bodi ya TCU yavunjwa kutokana na kupitisha majina ya wanafunzi wasiokuwa na vigezo. Bodi ya TCU yavunjwa kutokana na kupitisha majina ya wanafunzi wasiokuwa na vigezo. Reviewed by Unknown on 22:54:00 Rating: 5
Powered by Blogger.