WATENDAJI WATAKIWA KUHAKIKISHA USALAMA WA RASILIMALI ZA MISITU
EVELYN
MKOKOI
(Ofisi ya Makamu ya Makamu wa Rais Mzingira)
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu
wa Rais Muungano na Mazingira Mh. Luhaga Mpina, amewataka watendaji katika
ngazi za uteuzi nchini kushiriki kikamilifu katika kuhahikisha usalama wa
rasilimali za misitu.
Naibu Waziri Mpina ameyasema hayo leo
katika Pori la Ruvu Kaskazini ikiwa ni siku ya Kitaifa ya kupanda miti na
kueleza kuwa Serikali imekuwa na lengo la kupanda miti milioni moja nukta tano
(milioni 1.5) kwa mwaka mzima katika kila wilaya, na kuwataka watendaji waliopo
katika ngazi za uteuzi yaani Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri na Makatibu
wakuu, kuhakikisha lengo hili linafikiwa na kueleza kuwa viongozi watakaoshindwa kusimamia zoezi hili
majina yao yatapelekwa katika mamlaka za uteuzi na kuchukuliwa hatua, hii ikiwa
ni njia ya kupima usalama wa rasilimali hizi.
Akiongea na wananchi katika Pori la
Ruvu Kaskazini, Mh. Mpina alisema kuwa asilimia 61 ya ardhi ya nchi ipo kwenye
hatari ya kuwa jangwa kutokana na
uharibifu wa mazingira utokanao na ukataji miti ovyo, na takwimu zinaonyesha kuwa takribani hekta laki
tatu nukta sabini na mbili za misitu zinakatwa kila mwaka kwa matumizi mbali
mbali. “mikoa nane nchini iko hatarini kuwa jangwa”. Alisisitiza.
Akielezea athari, zitokanazo na uharibifu wa misitu, Mh. Mpina alisema taifa
linaweza kutumia mabilioni ya fedha kwa ajili ya kununua chakula kuwalisha wa
Tanzania kutokana na ukosekanaji wa mvua ,vyanzo vya maji kukauka, upatakinaji
wa umeme kuwa wa kusuasua kutokana na uharibifu wa misitu na vyanzo vya maji.
Kwa upande Mwingine Mh. Mpina alisema
kuwa serikali imekata miti kwa sababu mbalimbali za msingi ikiwa ni pamoja
ujenzi wa miundo mbinu kama vile barabara, reli ujenzi wa bomba la gesi, hivyo
basi kuna jukumu kubwa la kupanda miti mingi zaidi ya hiyo iliyokatwa.
Akitolea Mfano wa taasisi za huduma
ya misitu Nchini (TFS) iliyopo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii, Mh. Mpina aliainisha kuwa taasisi zote za
serikali zisaidie taifa kubainisha ni mazao gani ya misitu yanaweza kupandwa katika maeneo
gani kulingana na mahitaji ili kuweza kunusuru upotevu wa rasimali ya misitu.
WATENDAJI WATAKIWA KUHAKIKISHA USALAMA WA RASILIMALI ZA MISITU
Reviewed by WANGOFIRA
on
12:19:00
Rating:
No comments: