WARAKA KWA WANAZUONI NCHINI.

Na 
SHITINDI VENANCE.

KATIKA MAISHA YA CHUO.

Katika maisha haya wengi wanaishi maisha ya starehe na hii ni mahususi kwa watu wenye mkopo (boom), Lakini cha ajabu kundi hilihili hugeuka ghafla kama kinyonga na kuishi maisha magumu wakati pesa za boom zikiisha.  Kinapofika kipindi cha mwisho wa muda wa boom hilo na bahati mbaya zaidi kama boom linalofwata litacheleweshwa na bodi basi hali huwa mbaya zaidi kufikia watu kukomnika na wengine kupiga shato pori.

MAISHA BAADA YA CHUO.

Wengi  wanapojiunga na chuo kwa mara ya kwanza na kubahatika kupewa mkopo kutoka bodi ya mikopo, hujisahau na kuamini kuwa maisha ya kupewa mkopo ni ya milele na kamwe hayatakoma na hivyo kutumia pesa wanavyoona inawafaa. Lakini mwisho wa siku ujikuta wakiwa katika wakati mgumu na kuanza kuombaomba.

Waswahili husema hakuna marefu yasiyo na ncha, hufika pasipo hodi, ambayo nami nakubaliana nayo pasipo hata shaka. Hivyo ni wakati muafaka kwa wanazuoni kutengeneza nidhamu ya matumizi ya pesa wawapo chuoni maana maisha hubadilika ghafla.

Katika maisha mpya baada ya chuo huko mwanazuoni hujikuta hamiliki kitu chochote zaidi ya kompyuta pakata (PC) na radio maarufu kama sabufa.

Hapa hugutuka kuwa hana chumba cha kulala wala kodi ya kupanga, hana mtaji wa kuanza biashara wala biashara inayoishi, kifupi hana mbele wala nyuma, 
na matokeo yake atarudi nyumbani kwa baba na mama kuendeleza unyonyaji na utegemezi kwa wazazi aliowanyonya takribani miongo zaidi ya miwili ya maisha yake.
Swala hili linamadhala makubwa yasiyoonekana moja kwa moja kwa muhusika na jamii kwa ujumla, hii ni kwasababu

Kwanza mtu huyu atawakatisha tamaa wadogozake wengine na hata wanajamii kuwekeza katika ELIMU wakilejelea maisha magumu aishiyo mwanazuoni huyu, maisha ya utegemezi usiokoma ikilinganishwa na wale wasio na elimu kubwa.

Pili kulalama hovyohovyo kwa kukosa ajira kwa msomi huyu kutajenga picha mbaya kwa wanajamii kwamba ukisoma lazima uajiliwe na kama hutoajiliwa basi mambo yatakuwia vigumu na wengi wa wanajamii watajengeka katika mtazamo huo hasi katika karne ya 21.

Tatu mwanazuoni husika ataishusha hadhi ya mwanazuoni kutoka kuwa mtatuzi wa matatizo (problem solver) na kuwa muelezea matatizo kitu ambacho si dira ya elimu popote duniani.

WITO WANGU KWA WANAZUONI WENZANGU. 

Wanazuoni wote wakike kwa wakiume wanapaswa kutambua kuwa ndio taifa la Leo, na kila kifanyikacho kina matokeo kwa jamii  ambayo yawezakuwa hasi au chanya hivyo kuanzia sasa inapaswa kufanya mambo yafananayo na hadhi ya wanazuoni.

Pia inapaswa kujua fika kuwa pesa zitolewazo zinatosha, ikiwa mtu kujibana na kuanzisha miradi inayoweza kujiendesha yenyewe pasipo na usimamizi mkubwa kutoka kwa mhusika. na hivyo kujiingizia kipato katika maisha ya chuo na hata maisha baada ya chuo. Na kurudisha heshima ya mwanazuoni na hata kuliingizia taifa letu Mapato kupitia kodi.

Mwisho kuzaliwa masikini si kosa kosa ni kufa masikini, Mungu wabarikini sana mnapofanya maamuzi ya matumizi mazuri ya pesa za boom.

Waraka huu umeandikwa na shitindi Venance, waziri wa mikopo Udsm, waweza wasiliana kwa namba 0759704444 au 0676705440.
WARAKA KWA WANAZUONI NCHINI. WARAKA KWA WANAZUONI NCHINI. Reviewed by WANGOFIRA on 20:48:00 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.