NI KWELI DR.RIOBA ATAIBADILI TBC AU ATABADILISHWA NA TBC?
Unapozungumzia kuhusu tasnia ya habari, kamwe hauwezi kuacha kutaja mchango wa Dr. Ayoub Rioba ambaye hivi karibuni ameteuliwa kuwa Mkurugenzi mkuu wa Shirika la Utangazaji la Tanzania yaani TBC.
Uteuzi
huu umepongezwa na kupokelewa kwa mikono miwili na wadau mbalimbali wa habari.
Na wale wengine ambao wanauzoefu mkubwa wa kiuchambauzi ambao wanaiona TBC
imepewa mtu sahihi anayeweza kuifikisha mahali ambapo Shirika la Utangazaji na
la Umma linapaswa kuwa.
Binafsi
nitoe pongezi zangu za dhati kwa uteuzi huo ambao pasipo shaka yoyote kuwa Dr.
Rioba atatekeleza vyema majukumu yake pasipo kuwa na woga wowote. Kwani kauli
alizokuwa akizitoa kuhusiana na mienendo ya vyombo vya habari, sekta nzima ya
habari na jinsi vinavyoendeshwa. Ambapo wamiliki wa vyombo hivyo utumia nguvu
ya sema na propaganda kupindisha ukweli na kuwafanya waandishi wa habari katika
vyombo hivyo kuweka kando taaruma na kubaki kufuata matakwa yao.
Kwa
namna moja ama nyingine watu wamegawanywa na kuona baadhi ya vyombo vya habari ni
bora kuliko vingine. Na kuamini kuwa jambo fulani likitokea kituo X kitaripoti vizuri habari hiyo kuliko kitakavyo
ripoti kituo Y. na hata kama kituo X kikiripoti basi kutakuwa na walakini wa
taarifa hiyo.
Nakumbuka
maandiko ya Dr. Ayuob Rioba enzi zile anaandikia Raia Mwema, januari 30, 2013 aliandika
makala iliyokuwa na kichwa kinachosomeka “Changamoto za vyombo vya habari
katika demokrasia ya Tanzania” ambapo ililenga jinsi vyombo vya habari vya Tanzania
vinakumbana na changamoto nyingi kuanzia kwa waandishi kufanya kazi kwq
kuzingatia matakwa ya wamiliki na kutupilia mbali taaruma.
Nanukuu
maneno machache aliyoyaandika katika gazeti la Raia Mwema la siku ya Jumatanno
ya januari 6, 2013
“Katika demokrasia ya vyama vingi ambapo
panakuwa na uhuru wa mawazo, lakini pia vyombo mbalimbali vyenye umiliki
tofauti, si rahisi Serikali ikafanikiwa kumiliki au kuficha ukweli. Hivyo basi,
hata Serikali ikiamua kuendelea kutumia vyombo vyake vibaya kwa propaganda za
kudanganya umma, atakayedhalilika ni Serikali yenyewe na vyombo vyake kwa
sababu wananchi watajua ukweli kupitia njia nyingine”.
Ukweli
huu aliujua tangu zamani ambapo kwa kipindi hicho vyombo vya habari vya umma
ambavyo ni gazeti la Habari Leo, TBC1, TBC Taifa ambazo kwa kiasi kikubwa
utumiwa na umma mkubwa wa watanzania, vilikuwa vimepoteza mwelekeo.
Pia
ukirudi nyuma kidogo, mwaka jana kipindi cha uchaguzi pale Televisheni ya Taifa
ya TBC1, ilionyesha upendeleo wa wazi kwa chama tawala, kwa kuonyesha matangazo
ya moja kwa moja kutoka sehemu mbalimbali ambapo wagombea wa nafasi mbalimbali
wa chama tawala wakiwa majukwaani. Huku vyama vya upinzani vikiachwa pasipo
kuwa na mrejesho (coverage) yoyote kutoka televisheni ya taifa.
Ukizingatia
hayo ni juzi juzi tu ambapo TBC1 ilirusha moja kwa moja matangazo ya harusi ya
tajiri mmoja na kuacha mambo ya muhimu ambayo kama televisheni ilipaswa
kuonyesha. Itakumbukwa kuwa hata taarifa ya habari kwa siku hiyo haikuonyeshwa.
Kwa kile walichokidai kuwa mwenye harusi alilipia pesa nyingi za muda wa
maongezi.
Hiyo
ndiyo ilikuwa TBC ambayo kiukweli ilikuwa imepoteza dira na mwelekeo kama
televisheni ya taifa. Ambayo kila mwanasiasa hususani kutoka chama tawalaa
walitumia kutolea propaganda zao. Na kusahau kuwa wanaongozwa na kauli mbiu ya
“Ukweli na uhakika”
“Kwa
kweli ilikuwa inachekesha na mara nyingine kuhuzunisha jinsi ambavyo kituo hiki
kilikuwa kikiendeshwa kama kituo cha chama, maana TBC ilikuwa inakera na kutia
kichefuchefu kuiangalia maana ilikuwa imekoswa mwelekeo. Maana kulikuwa hamna
vipindi ambavyo vinavutia watu kuviangalia. Kulikuwa na kipindi maalum
kilichojulikana kama “This week in Perspective” kikaondolewa ambapo Dr. Ayoub
alikuwa mmoja wa waendesha mjadala. Alisema Amina Ramadhan mkazi wa Dar es salaam.
Kwa
upande wake Mhadhili wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM) ambaye pia ni
mwanasiasa na mshauri wa Chama cha ACT- Wazelendo Profesa Kitila Mkumbo
aliandika kwenye akaunti yake ya twitter kwa lugha ya kingereza kuwa
“Congratulation comrade Dr.Ayoub Rioba on your new appointment as TBC boss.
Please bring back This week in perspective programme” akiwa na maana kuwa
Hongera Dr. Ayoub Rioba kwa kuteuliwa kuwa Mkurugenzi mkuu wa TBC, nakuomba
urudisha kipindi cha This week in Perspective.
Lakini
pia bado naikumbuka makala yako ya januari 6, 2013 ambayo nimeielezea hapo juu,
uliandika jinsi chombo hiki cha Umma cha TBC kinavyotumiwa na wanasiasa na
wanahabari kutumikishwa kisiasa kuliko kutumia taaruma zao katika utekelezwaji
wa kazi zao. Uliandika
“TBC bado inaingiliwa na baadhi ya
wanasiasa ambao ama kwa kutokujua au kwa ubinafsi wao, wanaamini kwamba kile ni
chombo cha Serikali kama ilivyokuwa kwa Redio Tanzania (RTD). Wanashindwa
kubaini kwamba katika demokrasia ya vyama vingi, TBC huru ni bora zaidi na
inaweza kuifanya Serikali iaminike zaidi kuliko ile TBC inayokuwa inafugwa na
kuingiliwa na Serikali kinyume na matakwa ya taaluma.”
Sasa umeteuliwa Dr. Rioba kuwa
Mkurugenzi mkuu wa Shirika la utangazaji wa Taifa (TBC), kelele zote
ulizozipaza zimesikika na Rais ameamua kukuteua kuongoza taasisi hii muhimu
ambayo kwa sasa matumaini wengi yameanza kurejea kuwa huenda TBC ikarudi kama
ilivyoanzisha na kufanya kazi kama shirika la umma na kufanana na BBC ambalo ni
shirika la Utangazaji la Uingereza.
Nakumbuka pia makala aliyoiandika
katika gazeti la Raia mwema la januari 9 ikiwa na kichwa kinachosomeka “Dhima
ya vyombo vya habari katika demokrasia ya vyama vingi” ulieleza vyema na kwa
umakini wa hali ya juu jinsi wanazuoni mbalimbali wanavyoamini kuhusiana na
dhima za vyombo vya habari katika nchi yeyote ile inayofuata misingi ya demokrasia
uliandika maneno ambayo ni ya muhimu kwa vyombo vya habari kufanya kazi zao
pasipo kuingiliwa.
“Kwanza ni haki na
uhuru wa kila mtu kuwa na maoni, na kujieleza; pili, haki na uhuru wa
kuanzishwa/kuwapo kwa vyombo vya habari; tatu, haki na uhuru wa kufanya kazi ya
uandishi /uhariri wa habari bila kuingiliwa au kuzuiwa na mtu au taasisi yoyote
mbali na maadili ya kitaaluma ya uandishi; nne, haki ya kupata taarifa kutoka
serikalini isipokuwa tu zile ambazo kutolewa kwake hadharani kutaathiri maslahi
ya nchi na wananchi kwa ujumla (na maslahi haya ni lazima yafafanuliwe katika
katiba na si kuamuliwa na waziri husika); tano, mfumo wa uwajibikaji
unakaohakikisha kuwa vyombo vya habari na wanahabari wanatekeleza majukumu yao
kwa uhuru na kwa kuzingatia maadili ya taaluma yao; mwisho, sheria ndogo
zinazolinda haki na uhuru ulio katika katiba”.
Hizo ndo sifa ambazo vyombo vya
habari vinapaswa kuwa nayo katika nchi za demokrasia ikiwemo Tanzania. Ambayo
kwa siku za karibuni vyombo vya habari vimekuwa vikilaumiwa kwa wanahabari wake
kukosa weredi katika kazi zao.
Hamis Dambaya ambaye pia ni mmoja wa waandishi
nguli katika masuala ya siasa hapa nchini yeye anamuona Dr. Rioba kama
mwanahabari shujaa. Ambaye TBC anaimudu vyema kutokana na msimamo wake tangu
akiwa mwandishi wa habari chipukizi akiandikia gazeti la serikali la Daily News
miaka ile ya 1990.
Dambaya anamfahamu Rioba Vizuri
mbali na kufanya nae kazi kwa muda mrefu anamuelezea kitasnia zaidi kuliko
Kiuhadhiri. Anaeleza
“Mimi kama mwandishi wa habari
namuangalia Dr. Rioba kuwa ni mwandishi mahiri, asiye na uoga, na mwenye uwezo
wa kueleza hisia zake kwa jambo lolote lile bila kutafuna maneno”
Pia Dambaya anaeleza jinsi alivyokuwa
anavutiwa na Kolamu aliyojulikana kama “By the way” tangu akiwa anasoma na
kukumbusha kuhusu moja ya kichwa cha
habari kilichosomeka In rememberance of Bulugu ambapo alivyoeleza kwa kina
kuhusu umuhimu wa uandishi wa habari wa kujali maslahi ya umma na kusema wazi
kwamba kazi ya uandishi wa habari si kazi ya kufurahisha wakubwa bali kazi ya
kusaidia wanyonge ambao mara nyingi haki zao zimekuwa zikipotea.
Huyo ndiyo Dr. Rioba ambaye kwa
sasa anachangamoto kubwa ya kuubali mfumo wa TBC kuwa Televisheni ya taifa ili
sheria ya vyombo vya habari ikipitishwa vyombo vya habari vijiunge na TBC1,
katika habari ya saa mbili usiku na baadhi ya vipindi maalum ambavyo vinahitaji
busara za wamiliki wengine wa vyombo vya habari kukubaliana na Shirika la
Utangazaji la Taifa.
Ikumbukwe kuwa Dr.Rioba anaingia
wakati ambapo bado sakata la urushwaji wa matangazo ya moja kwa moja kutoka
bungeni yakiwa yamesitishwa kwa madai ya hukosefu wa pesa za kurushia matangazo
hayo. Jambo ambalo lilizua gumzo kubwa miongoni mwa wananchi na baadhi ya wadau
wa habari wakiwemo, Jukwaa la Wahariri Tanzania. Ambapo kwa upande wao
waliazimia kutafuta pesa za kuilipa TBC kurusha matangazo hayo moja kwa moja
kutoka bungeni Dodoma.
Huu ni mtihani mkubwa sana kwa Dr.
Rioba ambao si wa kuingia kichwa kichwa unahitaji maridhiano na kutumia busara
nyingi maana watanzania wametulia tu. Wanangoja Bunge lianze ndipo waone kama
ni kweli TBC imeamua kusitisha matangazo hayo kwa baadhi ya muda ili wayarekodi
na kuyarusha muda wa usiku katika kipindi kiitwacho Leo katika Bunge.
Nimtakie kila la kheri katika
ufanisi wa kazi ya Ukurugenzi namalizia kwa maneno machache ya Hamis Dambaya
aliyasema Rioba Twakuamini, wewe kijana makini, usilale asilani, Umma
wakutegemea, Rioba Tumia vipawa vyako kufanya mabadiliko. Huu mtihani kwako
utashinda nakwambia, Rioba- wavivu watakujia , majungu kukuambia , dawa ni
kupuuzia hapo utaendelea.
Mungu Ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika,
Mungu libariki Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) na watanzania wote.
Makala haya yameandikwa na
mwanafunzi wa mwaka wa Pili katika fani ya mawasiliano kwa umma, ya Chuo kikuu
cha Dar es salaam. Anapatikana kwa namba ya simu ya 0763580901, 0716216249 na
barua pepe ya barakangofira@gmail.com.
NI KWELI DR.RIOBA ATAIBADILI TBC AU ATABADILISHWA NA TBC?
Reviewed by WANGOFIRA
on
21:50:00
Rating:
No comments: