MAMBO TAYARI, HATMA YA DARUSO 2016/2017 MIKONONI MWA HAWA....
WAJUMBE WA TUME YA RUFAA YA UCHAGUZI WA DARUSO 2016/2017.
Kama
walivyochaguliwa na kikao cha mwisho cha bunge la Daruso jana 09/04/2016.
1. Alpha Abdallah
(SJMC)
2. Kiyagi
Steven (SoED)
3. Shitindi
Venance (CoSS)
4. Ibrahim Shija
(CoHU)
5. Kimario
Seraphin (CoICT)
6. Embas
Julius (CoNAS)
7. Asimwa Owakisha
(IKS)
8. Alexander
Mapunda (CoET)
9. Elihuruma Nyari
(UDBS)
10. Frank Katyega
(UDSoL).
Wajumbe hawa ndiyo watakaokutana kesho Jumatatu saa
nne kamili asubuhi kwaajili ya kufanya uchaguzi wa mwenyekiti na Katibu wa tume
ya rufaa ya uchaguzi.
Uchaguzi wa
mwenyekiti na Katibu wa tume hiyo unatarajia kuwa chini ya usimamizi wa Ofisi
ya Spika wa bunge la Daruso na Ofisi ya Mshauri wa wanafunzi (Dean of
students).
Majukumu makubwa
ya tume ya rufaa ya Uchaguzi wa Daruso ni kupokea rufaa zinazotokana na maamuzi
ya tume ya uchaguzi ya Daruso.
Kikatiba chombo
hiki ndicho chenye maamuzi ya mwisho juu ya mchakato wa uchaguzi wa Daruso hata
hivyo katika miaka ya hivi karibuni Tume ya rufaa ya uchaguzi imekuwa dhaifu,
isiyo na meno na isiyo na muda wa kutosha wa kushughulikia malalamiko
yanayopelekwa katika tume hiyo kutokana na ratiba ya uchaguzi kuibana Tume hiyo
na mara nyingine ikishughulikia malalamiko ilihali tayari uchaguzi umeingia
katika hatua zingine.
MAMBO TAYARI, HATMA YA DARUSO 2016/2017 MIKONONI MWA HAWA....
Reviewed by WANGOFIRA
on
13:12:00
Rating:
No comments: