CHADEMA; Mrudisheni Dr. Slaa kundini

Tuseme tu ukweli,Dr Slaa alikuwa nguzo kubwa ndani ya CHADEMA na UKAWA,tunamhitaji huyu mzee wa kukusanya nyaraka na kutoa matamko yenye facts tupu.Inaonekana wazi sasa hata CHADEMA hawajui wanasimama kwenye nini hasa!either kupinga ufisadi?hell no hawana huo ubavu kama mwanzo!Je kukosoa serikali ya Magufuli?pamoja na kukosoa tunakosoa hata utumbuaji majipu ambayo yalikomaa.
2020 kuna sera gani UKAWA CHADEMA watatumia?kama ni mabadiliko je kwa Magufuli hamna?utumbuaji majipu TRA,bandari,ndege 3 zinakuja,kiasi flani bila unafki Rais Magufuli anajitahidi ingawa kukosolewa ni kawaida.

Tumlaumu Magufuli kwa kukaa pembeni suala LA uchaguzi Zanzibar,na tuilaumu tume ya uchaguzi kwa kasoro za uchaguzi.

Ni mabadiliko gani UKAWA/CHADEMA tunahitaji hasa kwa sasa?Kujipanga kunahitajika sana!


Bado CHADEMA tunamhitaji Dr.Slaa,mtu ambaye anajua anachokisema,anajua anachokisimamia,chadema haitakiwi kutoa matamko ambayo hata wao wenyewe wanajifunga kwa kauli zao awali.

Ili UKAWA ipate miguu ya kusimama,kukosoa serikali,kufichua maovu ,kutoa tamko zenye kutikisa nchi na zenye facts ili Magufuli atumbue majipu vizuri bado inamhitaji Dr.Slaa.

Mheshimiwa Edward Lowasa hana credibility ya kutoa tamko,Mbowe bila Dr Slaa hana pia,misingi ya CHADEMA ilikuwa kwenye Dr Slaa 30%.

Tunamhitaji Dr.Slaa kuwa ndani ya CHADEMA ili akiongea kuwe na kipya maana akiwa pamoja na Mbowe ,Mnyika,Lissu,Msigwa n.k,wakipaza sauti kwa pamoja wanasikika na watanzania tunawaelewa.

Ili upinzani ukue Tanzania UKAWA NA CHADEMA tunamhitaji Dr Slaa,pia Dr.Slaa hawezi kusimama mwenyewe bila CHADEMA,hakuna chama aliyoijenga kama CHADEMA,nje na hapo hawezi kuaminika.

Viongozi wa UKAWA na CHADEMA washauriane wawe timu moja na Dr Slaa,wanamhitaji.

NAFUNGUA MJADALA
CHADEMA; Mrudisheni Dr. Slaa kundini CHADEMA; Mrudisheni Dr. Slaa kundini Reviewed by WANGOFIRA on 23:05:00 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.