WIZARA YA ELIMU KUANZA KUTATUA CHANGAMOTO ZA SOMO LA HISABATI.
Mkurugenzi wa Elimu ya sekondari kutoka wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Bi Paulina Mkonongo (wa nne kushoto) akiwa na viongozi wa Chama cha Hisabati Tanzania wakati wa maadhimisho ya siku ya PI duniani yaliyowafinyika uwanja wa Mnazi mmoja jijini Dar es salaam. (picha na Perus Benson)
Na, Mtapa Wilson
Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na
Ufundi imeahidi kuanza kutatua changamoto zinazopelekea ufaulu mbovu wa somo la
hisabati katika ngazi ya elimu ya msingi na sekondari.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Elimu ya
Sekondari kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi,Bibi Paulina
Mkonongo wakati akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati wa
maadhimisho ya PI duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja.
Bibi Mkonongo amesema kuwa somo la
hisabati ni muhimu sana kwani ni kichocheo muhimu katika maendeleo ya sayansi
na teknolojia ambapo sasa serikali ikiwa imejikita katika sera ya viwanda.
“Somo la Hisabati ndio malkia wa Sayansi
na Teknolojia. Tunahitaji sana wanafunzi
wasome somo la Hisabati ili kuweza kuendeleza Sayansi na Teknolojia ambayo
itasaidia katika utekelezaji wa sera ya viwanda amabyo inaonekana kuwa muelekeo
wa serikali yetu katika kukuza uchumi wa nchi”
“Tunawajibu wa kutoa semina elekezi kwa
walimu wa somo la hisabati. Lakini pia lazima wanafunzi lazima wahimizwe kusoma
hisabati kwa kuwekewa misingi bora itakayowasaidia kuepuka dhana potofu ya
kusema hisabati ni somo gumu”
Maadhimisho ya siku ya PI duniani
yaliadhimishwa kwa maonesho mbalimbali ya vifaa vya kujifunza somo la hisabati
kwa vitendo ambapo shule mbalimbali za msingi na sekondari zilishiriki.
WIZARA YA ELIMU KUANZA KUTATUA CHANGAMOTO ZA SOMO LA HISABATI.
Reviewed by WANGOFIRA
on
09:08:00
Rating:
No comments: