THAMANI YA MWANAHABARI KWA JAMII
NA,
BARAKA NGOFIRA
0763580901,
0716216249
Hakuna
shaka yoyote kuwa kuna mtu hajui umuhimu wa vyombo vya habari katika
kuhabarisha umma, na kufanya taifa lolote lile liweze kuwa na maendeleo
makubwa. Si tu maendeleo bali pia vyombo vya habari vimekuwa vikifanya kazi
kubwa ya kufichua maovu mbalimbali yanayotokea kwenye jamii zetu.
Rudi
nyuma kidogo wakati wa uchaguzi mkuu uliopita mwaka jana jinsi vyombo vya
habari vilivyofanya kazi kubwa ya kuhabarisha umma, kuhusu matukio yote na
wengine wakawa hawapitwi na lisaa hata limoja kabla hawajasikiliza redio,
kusoma gazeti au kutazama televisheni.
Hii
ni kuonyesha tu kuwa jamii ya sasa yetu haiwezi kuishi pasipo vyombo vya
habari, na kama kuna mtu anabisha ajaribu kujifungia kwa siku mbili chumbani
kwake asishike simu, asisikilize redio wala kusoma gazeti na wala kutazama
televisheni hapo ndipo atakapoelewa kile ninachokimaanisha.
Mbali
na kuwepo kwa mitandao ya kijamii ambayo imesaidia kusambaa za taarifa ambazo
mara nyingi huwa ni za uongo lakini bado umuhimu wa vyombo vya habari bado huko
palepale, tazama asubuhi watu wengi husema wanaamka na BBC, DW pia hawaachi
kusikiliza uchambuzi wa magazeti ya nyumbani katika redio na televisheni za
nyumbani.
Hapa
ndipo unaona jinsi vyombo vya habari vinavyofanya kazi kwa kusaidiana na jamii
kuibua na kufichua maovu yanayotokea ndani ya jamii zetu, vyombo vya habari kwa
sasa vimekuwa sehemu ya maisha ya wanajamii katika nchi yoyote ile duniani.
Piga
picha miaka ya 1980 taarifa mbalimbali za kiserikali zilikuwa zinawafikiaje
wananchi? Au watu walitambuaje kuwa hayati Baba wa Taifa Mwl.Nyerere anafanya
ziara kwenye maeneo yao? Lakini leo mambo ni tofauti kabisa kwani leo matukio
mengi yakitokea hasa ya kitaifa hurushwa moja kwa moja kwenye vyombo vya habari
hususani redio na televisheni.
Hapo
ndipo utajua kuwa vyombo vya habari vina umuhimu mkubwa kwa jamii yetu, lakini
cha ajabu na cha kushangaza taarifa au mambo mengi yanayofanywa na vyombo hivi
vya habari vinapendwa sana na vingi vinasifiwa lakini wanahabari hawapendwi.
Nasema
hawapendi kwa sababu maisha wanayoyaishi wanahabari ni tofauti kabisa na kazi
zao, wengi hudharauliwa, wanachekwa na kupuuzwa na baadhi ya watu na pengine
viongozi wa sekta binafsi na wale wa kiserikali.
Pia,
wanafunzi ambao wanasoma fani hizi nao hawapewi kipaumbele kwa kuambiwa kuwa
fani wanazosoma si kipaumbele kwa wao kupewa mkopo ili wasome na kubobea katika
fani hizi za habari. Hivyo ndivyo hali ilivyo.
Inashangaza
sana kuona mwanahabari mwanafunzi hananyimwa mkopo na pale anapoenda kuuliza
kwa nini amenyimwa mkopo na sifa na vigezo vyote anavyo. Jibu analopewa ni kuwa
fani anayosoma si kipaumbele cha yeye kupata mkopo wa kumuwezesha yeye kusoma
elimu ya juu.
Wakiwa
na maana kuwa kama mtu hana uwezo wa kujilipia ili asome fani zinazohusiana na
masuala ya habari basi inambidi abadili maamuzi aende fani nyingine ambazo ni
kipaumbele. Ikiwemo ualimu na nyingine ambazo kwa sasa watu wanaenda kusoma ili
mradi tu na wao wajulikane kuwa walisoma elimu ya juu na kuongeza idadi ya
wasomi tena wengine wakiwa na shahada za juu. Lakini walichokisoma hawakijui
kwani haikuwa dhumuni lao kusomea fani hizo.
Kwa
hili inabidi serikali iliangalie kwa makini kwani inachangia kwa kiasi kikubwa
kukosekana kwa watu mahili na wanahabari machachali ambao wangesaidiana na
serikali pamoja na wananchi ili kujenga nchi yetu ili iweze kuwa na uchumi
imara na wenye kuleta tija kubwa kwa wananchi wa nchi yetu.
Kwa
hili pia nimuombe waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa, na Michezo Bwana Nape
Nauye, kwani ni jukumu lake kututetea kama waziri wa Habari, na kama ukishindwa
mtetezi mwingine hatuna. Tupiganie na ututetee maana ukishindwa wewe kama waziri
mwenye dhamana basi hatujui ni nani hatatutetea.
Najua
waziri huyu anafahamu fika kuwa wanafunzi wanaosoma fani hizi za habari
hawapewi kipaumbele cha kupata mkopo kwa ajili ya wao kusoma fani hizi za
habari. Kwa kuambiwa kuwa fani wanazozisoma si kipaumbele na hapa ndipo nabaki
na maswali mengi ya kujiuliza iweje wanahabari si vipaumbele na habari iwe
kipaumbele?
Inashangaza
sana mtu kutothaminiwa lakini kazi yake kuthaminiwa na kupewa kipaumbele,
tazama kazi wanazozifanya waanahabari, wanawafanya wanasiasa kuwa maarufu na
kuwajengea majina makubwa. Lakini wanahabari wakiwa bado hawathaminiwi, wala
kusikilizwa na wanasiasa hawa ambao washajengewa majina na vyombo vya habari.
Ni
ombi langu kwa waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bwana Nape Nauye
utusaidie, utupiganie na umshawishi waziri wa Elimu na mama yetu Prof.
Ndalichako ili nasi tupewe kipaumbele katika mwaka ujao wa masomo la sivyo,
Taifa letu litakuja kujuta miaka ya mbeleni kwa kukosa wanahabari mahiri na
waliobobeaa kwenye fani hii.
Kwani
ni jambo la aibu tena kubwa kwa nchi yetu kuona baadhi ya vyombo vya habari
kuendelea kufanya madudu ambayo kiukweli unabaki kujiuliza ni kweli watu hawa
wana taaruma ya habari au la? Kwani ni
aibu kabisa hata kusema hadharani kuwa mimi ni mwanahabari.
Na
kufanya taaruma yetu ya habari watu wengi kuiona kama ni ya watu wambea ambao
ni wenye kufuatilia maisha ya watu. Na baadhi yetu kudharauliwa na kuitwa
wadaku. Jambo ambalo ni aibu kubwa lakini ni kwa sababu tu baadhi ya wenzetu
ambao naamini hawanaa taaruma hii wanafanya kazi hizo za udaku.
Mwisho
ni ombi langu kwa wadau na wanahabari wote tuunganishe nguvu zetu pamoja
tuiombe
serikali yetu tukufu ituangalie kwa jicho la pili na watufanye nasi
tuwe kipaumbele kama zilivyo fani nyingine kama Ualimu, masomo ya Afya na fani
nyingine kwani umuhimu wetu ni sawa kabisa na tunategemeana na fani hizo na pia
tunatumika kama daraja la kupitishia taarifa mbalimbali.
Kwa
hiyo ni jukumu letu kama wanahabari kuunganisha nguvu na kuisisitiza serikali
ambayo naamini ni sikivu kwani nakumbuka hata Rais wetu Magufuli alituahidi
kuwa tuunde chombo ambacho atakutana nacho ili kujadili kero na ambazo
tunakabiliana nazo ambazo hata kutopewa kipaumbele katika elimu ya juu likiwa
moja wapo.
Makala
haya yameandikwa na mwanafunzi wa Shule Kuu ya Uandishi wa Habari na
Mawasiliano kwa Umma ya Chuo kikuu cha Dar es salaam. Anapatikana kwa
mawasilano ya 0763580901, 0716216249 na barakangofira@gmail.com.
THAMANI YA MWANAHABARI KWA JAMII
Reviewed by WANGOFIRA
on
04:13:00
Rating:
No comments: