NAIBU WAZIRI WA MIUNDOMBINU NA USAFIRISHAJI UDSM APIGWA RISASI, AFARIKI PAPO HAPO.
Naibu
waziri wa miundombinu na usafirishaji chuo kikuu cha Dar es salaam ambaye pia
ni mwanafunzi wa mwaka wa nne katika chuo kikuu hicho Bw. Mutaengerwa Mafwiri,
amefariki dunia baada ya kupigwa risasi na watu wanaosadikika kuwa ni
majambazi, katika eneo la Ubungo Msewe.
Mashuhuda
wa tukio hili wanaeleza kuwa marehemu amefikwa na mauti hayo mara baada ya
kutoka nje kwa ajili ya kwenda kushangaa kitu kilichozaniwa kuwa ni mlipuko wa
transfoma ndipo alipofyatuliwa risasi na majambazi ambao walikuwa wanapora na
kuvamia maduka yaliyo maeneo ya Ubungo Msewe.
Wangofira
Blog inaendelea kufuatia undani wa tukio hili kwa vyombo vya ulinzi na usalam
ili kujua ni hatua zipi zinafuata ili kuaga mwili wa marehemu na kuusafirisha
kwao kwa mazishi.
Ikumbukwe
kuwa hii si mara ya kwanza kwa wanafunzi wa chuo kikuu cha dar es salaam
kuuwawa kwa kupigwa risasi na matukio mengine kama wanafunzi kufa kwa kugongwa
na magari pale wanaporudi maeneo walipopanga, kwani mwaka jana wanafunzi wawili
wa chuo kikuu hiki pia waliuwawa kwa kupigwa risasi na wengine kujeruhiwa wiki
mbili zilizopita maeneo ya mabibo hosteli.
MUNGU
AILAZE PEMA ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA, AMENI.
-
NAIBU WAZIRI WA MIUNDOMBINU NA USAFIRISHAJI UDSM APIGWA RISASI, AFARIKI PAPO HAPO.
Reviewed by WANGOFIRA
on
13:28:00
Rating:
R.I.P KIONGOZI WETU
ReplyDelete