TANGAZO LA KAZI WIZARA YA KILIMO NA UVUVI
JAMHURI
YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA
YA KILIMO CHAKULA NA USHIRIKA
TANGAZO LA NAFASI ZA
KAZI
Katibu
Mkuu Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika anawatangazia Watanzania wote wenye
sifa zilizoanishwa hapa chini watume barua za maombi ya kazi zifuatazo.
1. Afisa Utafiti Kilimo Daraja la II
(Agricultural Research Officer II) Nafasi 70
(a) Sifa
za waombaji
Wawe wamehitimu Shahada ya Kilimo (Bsc
Agriculture General), Uchumi Kilimo, Uhandisi Kilimo, Food Science and Technology,
Biotechnology Laboratory Sciences, Agronomy,Bsc Environmental Science na Horticulture kutoka chuo kinachotambuliwa
na Serikali.
(b) Majukumu
Ø
Kusaidia
kukusanya na kuandika ripoti za utafiti chini ya maelekezo ya Afisa Utafiti
Kilimo Mwandamizi.
Ø
Kukusanya,
kurekodi na kuchanganua takwimu za kazi za Utafiti zinazoendelea.
Ø
Kusaidia
katika kuendesha semina na kuwaelekeza wakulima jinsi ya kutumia teknolojia
mpya kwa kuzingatia hali ya uchumi na
mazingira yake.
Ø
Kutoa
ripoti ya maendeleo ya Utafiti na mapendekezo ya Utafiti katika Mikutano ya
kanda.
Ø
Kufanya
shughuli za Utafiti chini ya maelekezo na uangalizi wa Afisa Utafiti Kilimo
Mwandamizi.
Ø
Pamoja
na kazi nyingine za Utafiti kama
atakavyopangiwa na kiongozi wake wa kazi.
(c) Mshahara
Ø
Mishahara
ya Watumishi wa Serikali ngazi ya TGRS A.
2.
Mhandisi Kilimo Daraja la II (Agro
Engineer II). Nafasi 88
Waombaji
watakaochaguliwa watapangiwa kazi Wizara ya Kilimo chakula na Ushirika na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).
(a)
Sifa za waombaji
Ø
Wawe
wamehitimu Shahada ya Uhandisi yenye mwelekeo mkubwa katika fani ya Kilimo,
Umwagiliaji,Ujenzi,Ufundi na Mazingira kutoka Chuo Kikuu kinachotambuliwa na Serikali
(b)
Majukumu
Ø
Kuandaa
program za mafunzo kwa wakulima kutumia zana za Kilimo
Ø
Kushirika
katika kufundisha wakulima na matumizi bora ya zana.
Ø
Kushiriki
katika ujenzi wa miradi ya Umwagiliaji
Ø
Kushiriki
kutengeneza michoro/ramani za umwagiliaji.
Ø
Kukusanya
takwimu za miradi ya umwagiliaji
Ø
Kufuatilia
program za mafunzo ya wanyamakazi mafundi wa matrekta wa wakulima jinsi ya
matumizi ya wanyama kazi na matrekta
Ø
Kushiriki
kuratibu na kutoa huduma za umwagiliaji pamoja na matumizi ya maji.
Ø
Pamoja
na kazi zingine atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi.
Ø
Kupitia
mapendekezo ya miradi mbalimbali ya ufundi yanayowasilishwa Wizarani.
Ø
Kusimamia
mikataba ya ujenzi/ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji.
Ø
Kushirikiana
na mafundi sanifu kuwafundisha wakulima uendeshaji wa skimu za umwagiliaji
(c)
Mshahara
Ø
Mishahara ya Watumishi wa Serikali ngazi ya TGS
E.
3.
Afisa Kilimo Daraja la II (Agro –
Officers II) Nafasi 378
Waombaji
watakaochaguliwa watapangiwa kazi Wizara ya Kilimo chakula na Ushirika na
Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).
(a)
Sifa za waombaji
Ø
Wawe
wamehitimu Shahada ya Sayansi Kilimo (Bsc.Agriculture General,Bsc.Horticulture,Bsc.Agronomy,Bsc.Environmental
Sciences) na Mazingira kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine au vyuo vingine
vinavyotambuliwa na Serikali.
(b)
Majukumu
Ø
Kudhibiti
visumbufu vya mazao na mimea
Ø
Kukusanya
takwimu za bei za mazao kila wiki na kila mwezi
Ø
Kukusanya
takwimu za upatikanaji wa mazao katika masoko kila wiki/mwezi
Ø
Kuendesha
mafunzo ya wataalamu wa Kilimo
Ø
Kufanya
ukaguzi wa ubora na matumizi ya pembejeo na zana.
Ø
Ufuatiliaji
wa mwenendo wa soko la mazao ya biashara
Ø
Kuendesha
mafunzo juu ya hifadhi bora ya udongo na maji
Ø
Kutoa
habari juu ya teknolojia mpya kwa wadau
Ø
Kuandaa/
kuandika taarifa za utekelezaji kwa sekta ndogo ya mazao.
Ø
Kusimamia/kuendeleza
taaluma ya uzalishaji mboga, matunda, maua na mazao mengine.
Ø
Kusimamia/kuendeleza
uzalishaji wa mbegu bora
Ø
Kuandaa,
kutayarisha, kufunga na kusambaza mbegu bora
Ø
Kufanya
ukaguzi wa mbegu mpya kwa kushirikiana na Watafiti wa mbegu kabla kupitishwa
Ø
Kuendesha
mafunzo ya kuzalisha mbegu matunda, maua na viungo
Ø
Kuhamasisha
uzalishaji wa mazao ya bustani
Ø
Kufanya
utafiti mdogo mdogo wa mazao yanayofaa kulimwa katika sehemu ya Kilimo cha
Umwagiliaji.
Ø
Kufanya
utafiti wa udongo
Ø
Kuhamasisha
uanzishaji wa vikundi vya wakulima/ wamwagiliaji
Ø
Kuzalisha
mbegu za msingi baada ya kuzalishwa na watafiti
Ø
Kuendesha/kusimamia
vishamba vya majaribio vya mbegu na uchunguzi maabara ili kuondoa utata juu ya
mbegu.
(c)
Mshahara
Mishahara ya Watumishi wa Serikali ngazi ya TGS
D.
4.
Mkufunzi Kilimo Daraja la II
(Agricultural Tutor II) Nafasi
38
Waombaji watakaochaguliwa watapangiwa kazi ya
kufundisha katika vyuo vilivyo chini ya Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika na
Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi.
(a) Sifa za waombaji
Wawe wamehitimu Shahada ya kwanza
yenye mwelekeo wa Kilimo (Bsc.Agriculture General,Bsc.Agricultural Engineer,Bsc. Agronomy,
Bsc.Irrigation Engineer) kutoka Chuo
Kikuu cha Kilimo- Sokoine au Chuo kingine kinachotambuliwa na Serikali.
(b) Majukumu
Kufundisha kozi za
stashahada na astashahada za kilimo nadharia na vitendo
Ø
Kuandaa
mtiririko na mpangilio wa masomo (Lesson Sequences and Plans)
Ø
Kusoma
na kuelewa vema mihutasari ya mafunzo na kuitafsiri kwenye masomo
Ø
Kuandaa
na kufundisha kozi za wakulima
Ø
Kuandaa
na kupanga somo la vitendo na kusimamia wanachuo wakati wa kujifunza
Ø
Kupima
maendeleo ya wanachuo kwenye mitihani kwa kipindi chote kinachohusika na
kutunza alama zao.
Ø
Kupima
maendeleo ya wanachuo kwa kushirikiana na Maafisa Kilimo wa Wilaya/Viwandani
wakati wa mafunzo kwa vitendo (Field Practicals).
Ø
Kutekeleza
shughuli nyingine za kikazi kadri atakavyopangiwa na Mkuu wake wa kazi.
(c) Mshahara
Ø
Mishahara
ya Watumishi wa Serikali ngazi ya TGS D.
Waombaji
wote katika barua zao ni lazima waonyeshe sehemu ambayo wangependa kupangiwa kwa
nafasi zile zinazohusisha zaidi ya wizara moja. Hata hivyo uamuzi wa mwisho juu
ya vituo ni wa mwajiri/ Mamlaka za ajira ambako nafasi zinapatikana.
\
MAMBO YA KUZINGATIA
Barua
za maombi ziambatane na Curriculum Vitae (CV), picha ndogo mbili ukubwa wa
pasipoti, cheti cha kuzaliwa, vivuli vya vyeti vya kuhitimu elimu ya sekondari
na Shahada husika .
Waombaji
wawe na umri usiozidi miaka 45.
Wahitimu walioajiriwa Serikalini hawaruhusiwi kuomba nafasi hizi
kwasababu tayari wana ajira
Wahitimu waliotuma maombi yao
kabla ya tangazo hili wanashauriwa kutuma maombi upya.
Barua zote za maombi ziwasilishwe katika
muda wa siku 14 kuanzia
tarehe
ya kwanza ya kuonekana tangazo hili.
Tangazo
hili linapatikana pia kwenye tovuti ya Wizara, www.kilimo.go.tz
Barua
za Maombi zitumwe kwa:
Katibu Mkuu,
Wizara ya Kilimo Chakula na
Ushirika,
S.L.P. 9192,
DAR
ES SALAAM.
TANGAZO LA KAZI WIZARA YA KILIMO NA UVUVI
Reviewed by WANGOFIRA
on
07:45:00
Rating:
No comments: