IJUE ZANZIBAR NA UTALII WAKE

Image result for picha za zanzibar

     
Image result for picha za zanzibar


Image result for picha za zanzibarImage result for picha za zanzibar
Image result for picha za zanzibar
Na, baraka Ngofira
 0763580901


Mji mkongwe wa Zanzibar ni mji wenye historia kubwa na jina kubwa sana hasa kwa kusifika katika biashara ya utumwa ambapo kulikuwa na soko kuu la Afrika Mashariki la kuuzia watumwa kutoka katika nchi zinazozunguka Afrika ya mashariki.
 Historia haiishii kutaja tu kama mji huu ni maarufu katika uuzaji na usafirishaji wa watumwa bali pia mji huu unasifika kwa kuwa na watu wengi maarufu ambao kusahaulika katika historia ya dunia ni vigumu kama vile sultan Seyyid Said, Tippu Tip, Siti binti Said ambaye alivuma kwa uimbaji wa taarabu za Kiswahili, pia wapo Shekh Abdallah saleh Farsy ambaye ni mwandishi wa vitabu maarufu na mtafsiri wa Quran katika lugha ya Kiswahili.
Mji huu mkongwe wa Zanzibar sio tu unasifika kwa historia ndefu bali pia ni mji ambao umeingizwa kwenye urithi wa dunia ukiwa na fukwe nzuri za kuvutia, maboma ya kuvutia na yaliyojaa maajabu ikiwemo jumba linalofahamika kama Beit-al-ajaib katika lugha ya kiarabu umaajabu wa jumba ili ni kuwa na nguzo 44 zilizojengwa  kwa umahiri na umaridadi na uimara wa hali ya juu.
Jambo la kufurahisha na kuvutia katika jingo hili ndilo jengo la kwanza Afrika Mashariki na kusini mwa jangwa la sahara kuwa na umeme na lifti, na hivyo kulifanya kuwa jumba la kitalii linalovutia watalii na watu wengine wafikao Zanzibar kwenda kutalii na kutazama jengo hili.
Pia limekuwa kivutio kikubwa kwa watalii kuja kujifunza tamaduni na mambo ya kale na hatua mbalimbali za kimaendeleo zilizo kuwa zikifanyika Zanzibar kwa kale na zinazo endelea mpaka sasa, kwa kweli ufikapo Zanzibar usisite kutembelea kwenye jengo hili la kimaajabu.
Kivutio kingine kinachovutia watu kwenda kutalii Zanzibar ni mji mkongwe wa Zanzibar mji wenye historia kubwa na jina kubwa duniani , mji uliokaliwa na watu wengi, mji wenye majumba mengi ya kitalii , makanisa na misikiti ya kihistiroria yote yanapatikana kwenye mji mkongwe wa Zanzibar.
Nyangumi nao wamekuwa kivutio kikubwa hasa kwa watalii watokao bara na nchi nyingine kuja kupiga picha nyangumi wanaoruka na kuonekana kwa uzuri wakitokea majini na kisha kutumbukia majini. Nyangumi hawa wamewavutia maelfu ya watalii kutembelea Zanzibar na kujionea kwa macho yao na wwengine kubaki midomo wazi wakiwashaa nyangumi hawa jinsi warukavyo na kutumbukia majini, kwa kweli Mungu aliumba ndiyo maneno ambayo uwatoka mara nyingi watu hawa.
Ukiachilia mbali nyangumi uwepo wa fukwe nzuri za kuogelea na kupumuzikia za Kendwa,Mungwi,na kiwengwa ni fukwe nzuri za kuvutia zinazokusanya watu wengi hususani nyakati za jioni na nyakati za sikukuu kama vile za Maulid na zile za Xmass na mwaka mpya . sio tu ni fukwe nzuri pia zina upepo mwanana unaowavutia watu wapate fursa hii hadhimu ya kukaa na wale wawapendao na muda mwingi kubadilisha mawazo.
Pia magofu ya kihistoria , chochoro nazo ni vivutio vikubwa hasa kwa wilaya ya mjini Magharibi ambapo watarii hutumia fursa hii adhimu kutembelea na kushuhudia majengo haya na magofu yaliyojengwa kwa umahili na umaridada na mpaka leo yanahifadhiwa vizuri ili kuendelea kuwavutia watu wote wanaotembelea Zanzibar.
Pia uwepo wa Kima wekundu wanaopatikana kwenye misitu ya Jozani na Ngenzi nao wamekuwa kivutio kikubwa sana hasa kwa watalii wanaofika kutembelea katika misitu hii ya ajabu kujionea wanyama hawa ambao ni adhimu kupatikana bara na katika misitu mingine iliyopo bara na katika nchi nyingine duniani. Kweli maajabu ya kima hawa na rangi zao zimekuwa kivutio kikubwa sana. Uwaangaliapo na hata kupiga picha za kwenda kuonesha watu ambao hawajawahi kuwaaona kima hawa na maajabu yao.

IJUE ZANZIBAR NA UTALII WAKE IJUE ZANZIBAR NA UTALII WAKE Reviewed by WANGOFIRA on 07:58:00 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.